Tigo yawekeza kuunganisha watu wa vijijini na kuboresha huduma zake.
Diwani
wa kata ya Bulyanhulu Bw. Joseph Makoba akikata utepe kuzindua minara
mipya ya kampuni ya simu za mkononi Tigo kata za Kakola na Segese
wilayani Kahama mkoani Shinyanga, anayeshuhudia ni meneja wa Tigo kanda
ya Ziwa Bw.Joseph Mutalemwa.
Tigo
Tanzania leo wanaendeleza mipango yao ya kuwekeza katika upanuzi wa
mtandao wake katika Kata za Kakola na Segese wilayani Kahama Mkoani
Shinyanga ili kuongeza kiwango cha ubora na upatikanaji wa mtandao huo
nchini kote. Upanuzi huo pia utakwenda sambamba na kujenga miundombinu
mipya ya mawasiliano hasa katika maeneo ya vijijini, kuleta mawasiliano
kwa maelfu ya watu. Minara mipya ya mawasiliano itajengwa nchi nzima
ambapo mradi huo umeanzia katika mkoa wa Kigoma na kuendelea maeneo kama
Mwanza, Tabora, Mara na Kagera.
Akitangaza
mradi huo, Meneja Mkuu wa Tigo Bw. Diego Gutierrez alisema “Tigo
Tanzania imeendelea kukua kwa kasi mwaka hadi mwaka. Bidhaa zetu za
kipekee na huduma pamoja na kuongezeka kwa wateja ni ushahidi wa wazi
kabisa wa kukua kwetu. Uzinduzi wa minara hii mipya utawezesha kuwapatia
wateja wetu bidhaa bora za kipekee zilizobuniwa katika ubora wa hali ya
juu ili wateja wetu waweze kunufaika na huduma na bidhaa zenye kiwango
cha hali ya juu kabisa kwa hatua mpya. Hii ndio dhamira yetu ambayo
imetufanya tuendelee kuwa kampuni inayoongoza ya mtandao wa simu za
mkononi Tanzania.”
Tukiwa
tayari na mtandao imara wa mawasiliano katika mikoa mingi ya Tanzania
bara na Zanzibar, upanuzi huu wa mtandao wetu unalenga kuhakikisha kuwa
mtandao wetu unapatikana katika mikoa mingi zaidi nchini. Itaboresha
ubora wa mtandao katika maeneo ambayo tayari yana mtandao wa Tigo
kuhakikisha mawasiliano yanaboreka zaidi na huduma za Intaneti
zinapatikana vizuri zaidi na wakati huo huo kuhakikisha kuwa tunapeleka
huduma za mtandao wa Tigo nje kidogo ya Tanzania, kuwawezesha wateja
wapya kuungana na wenzao ulimwenguni na kuwa sehemu ya jamii kubwa ya
mtandao wa mawasiliano ya simu.
“Tukiwa
tunajiamini katika utoaji wa huduma bora za mawasiliano ya simu na nia
ya kuendelea kusonga mbele zaidi kwa siku zijazo, tumeona umuhimu wa
kupanua na kuboresha mtandao wetu. Uzinduzi wa minara hii mipya
utatuwezesha kupanua huduma zetu za mawasiliano katika maeneo haya
mapya, kwa wateja tulionao na tutakaokuwa nao kama tunavyodhamiria”
Awali upanuzi wa mtandao wa Tigo vijijini ulianzia kata za wilayani Kasulu mkoani Kigoma
Katika
ripoti ya hivi karibuni ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ya
robo mwaka ya mawasiliano ya mwezi Septemba 2012, idadi ya wateja wa
Tigo iliongezeka kwa 20% kati ya mwezi Juni mwishoni 2012 na Septemba
30, 2012 ikiwa na wateja 630,000 walioripotiwa. Tukiwa na mikakati hii
ya upanuzi, tunatarajia kukua zaidi kwa mwaka huu 2013.
Comments