Rais Kenyatta azuru Uganda. Kunani?
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
amesafiri hii leo kwa ziara rasmi ya siku tatu nchini Uganda. Hii ni
ziara ya kwanza ya rais huyo katika nchi jirani ya Uganda tangu kuchukua
uongozi wa taifa hilo katika uchaguzi uliofanyika miezi mitatu
iliyopita.
Rais Kenyatta anafanya ziara hii kwa mwaliko wa
rais Yoweri Museveni ambaye alikuwa Kiongozi wa pekee wa taifa ya nje
aliyetoa hotuba katika sherehe ya kuapishwa kwa Uhuru Kenyatta, ambapo
alikemea mahakama ya kimataifa ya Uhalifu ICC kwa kuwalenga viongozi wa
Afrika katika oparesheni zake.
Rais Kenyatta na naibu wake wamefunguliwa
mashtaka katika mahakama hiyo ya ICC ya kuhusika na machafuko ya baada
ya uchaguzi nchini humo mwaka wa 2008.
Rais Museveni ni mmoja wa vingozi wa Afrika
wanaopinga mahakama ya ICC akisema kuwa inalenga kuwadhulumu waafrika
kauli iliyotolewa na viongozi wa Afrika walipokutana kwenye mkutano wa
mataifa ya Afrika au AU mjini Addis Ababa Ethiopia ambpo waliikemea sana
mahakama hiyo.
Kwa sasa haijulikani ikiwa swala la ICC litakuwa kwenye ajenda ya mkutanao wa viongozi hao..
Comments