BARAZA LA MADIWANI KILOLO LAAGIZA WAUGUZI WANAO KODISHA AMBULENCE NA KUPOKEA POSHO KWA MGONJWA HOSPITAL TEULE YA ILULA KUCHUNGUZWA ........

 watumishi  wa Halmashauri ya  Kilolo mkoani Iringa  wakiwa  wamesimama  kwa maombi ya kumkumbuka aliyekuwa  mkurugenzi  wao marehemu Mohamed  Gwalima
 Madiwani  wakimkumbuka  aliyekuwa mkurugenzi  wa Kilolo na diwani wa kata ya Ukumbi

 Diwani mteule wa kata ya  Ng'ang'ange  wilaya ya  Kilolo Msuva (kushoto) akila  kiapo mbele ya  mwenyekiti wa Halmashauri ya  Kilolo Joseph Muhumba leo anayeshudia wa  pili kulia ni kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya  Kilolo Benson Kilange
 Mbunge  wa  jimbo la Kilolo Prof Peter Msolla kulia akishuhudia zoezi la kuapishwa  diwani mteule wa kata ya Ng'ang'ange  leo
 Kiapo  cha utii  kwa  diwani mteule

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya  Kilolo JOseph Muhumba  akifungua kikao cha baraza la madiwani leo
BARAZA la madiwani katika  Halmashauri ya  Wilaya ya Kilolo mkoani  Iringa limeagiza kufuatilia  tuhuma  zilizotolewa na mmoja kati ya madiwani  wa baraza  hilo kuhusiana na Hospital  teule  ya Ilula  Ilula kuwakodisha  gari  la  wagonjwa (Ambulence) wagonjwa  wanaopewa  rufaa kwenda  Hospital ya mkoa pamoja na kuomba posho ya Tsh 10000 kwa mgonjwa .

Hatua  hiyo  imekuja kufuatia madai  yaliyotolewa na diwani Anna Kulanga kuhusiana na mwenendo  usiofaa unaofanywa na  uongozi  wa Hospital  hiyo teule ya  Ilula kwa kuwakodisha Ambulence wagonjwa.

Diwani  Kulanga alisema kuwa hatua  iliyofikiwa katika  Hospital  hiyo si nzuri kwani  siku za hivi karibuni walipata  kukodisha  Ambulence  hiyo kwa majeruhi wa ajali ambae alitakiwa kukimbizwa katika  Hospital ya Rufaa ya  mkoa wa  Iringa ila mbali ya majeruhi  huyo kupoteza maisha njiani ila bado  wauguzi  wawili waliomsindikiza majeruhi  huyo  walitaka  ndugu  kulipa gharama ya Ambulence  kiasi cha  Tsh 40000 pamoja na kuwalipa posho ya Tsh 20000 wauguzi  wawili  walioongozana na majeruhi  huyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI