NMB YAFADHILI SEMINA YA MAAFISA MAENDELEO WA VIJANA NCHINI

Benki ya NMB imefadhili semina kubwa iliyohusisha maafisa maendeleo wa vijana kutoka nchi nzima.Semina hii ambayo ilikua ni ya siku mbili ilifanyika katika kumbi za uwanja wa Taifa  jijini Dar es salaam. Mhe. Dkt.Fenera Mukangara ambae ni Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo  alizindua rasmi semina hii na kuishukuru Benki ya NMB kwa ufadhili mkubwa ambao wamejitolea ili kufanikisha semina. Dhumuni la semina ni  kujadili maendeleo ya vijana kuanzia ngazi ya halmashauri,kuimarisha utendaji kazi kwa vijana wa mikoa na wilaya.
 Mhe. Dkt. Fenera Mukangara ambaye ni Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo  akiongea na maafisa maendeleo ya vijana nchini wakati wa uzinduzi wa semina ya siku mbili.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari ,Vijana,Utamaduni na Michezo  Bw. Seth Kamuhanda akifafanua  jambo wakati wa semina hiyo.
Meneja wa NMB Mikopo Midogo Midogo Bw. Mashaga Changarawe akielezea huduma mbali mbali   zitolewazo na Benki ya NMB zikiwemo akaunti pamoja na mikopo mbalimbali kwa wajasiliamaliMeneja Mawasiliano  wa NMB, Josephine Kulwa akizungumzia jinsi ambavyo Benki ya NMB kwa kupitia huduma zake kwa wajasiliamali inavyosaidia kuongeza ajira kwa vijana nchini
Erick Shigongo nae alitoa maada kuhusiana  mafanikio na kujitambua katika ajira.
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI