KAMATI ZA MAADILI WANACHAMA WA TFF
Wanachama
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wanatakiwa kufanyia
marekebisho katika katiba zao kwa kuingiza ibara ya Kamati za Maadili.
Maagizo
hayo yanatokana na kikao cha Kamati ya Utendaji ya TFF iliyoketi
Novemba 23 mwaka huu jijini Dar es Salaam chini ya Mwenyekiti wake, Rais
Jamal Malinzi ambapo pamoja na mambo mengine ilijadili umuhimu wa
wanachama wake kuunda kamati hizo.
Wanachama
wa TFF ambao muda wao wa uchaguzi umekaribia, wanatakiwa kufanya
marekebisho hayo kwanza kabla ya kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi.
TFF ina aina tatu za wanachama. Wanachama hao ni vyama vya mpira wa miguu vya mikoa, vyama shiriki na Klabu za ligi Kuu.
FAINALI YA KOMBE LA UHAI CHAMAZI
Mechi
ya Fainali ya michuano ya Kombe la Uhai inayoshirikisha timu za umri
chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu itachezwa keshokutwa (Jumapili)
kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar
es Salaam.
Coastal
Union ndiyo itakayocheza fainali hiyo kuanzia saa 9.30 alasiri dhidi ya
mshindi wa mechi ya nusu fainali ya pili kati ya Yanga na Mtibwa Sugar
inayotarajia kuchezwa baadaye leo.
Mechi
ya fainali itatanguliwa na ile ya kutafuta mshindi wa tatu kati ya Azam
na timu itakayoshindwa katika mechi ya pili ya nusu fainali ya michuano
ya mwaka huu iliyoanza katika viwanja vya Karume na DUCE kabla ya
kuhamia Chamazi.
Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Comments