Bendi
ya Mlimani Park Orchestra almaarufu kama Sikinde inategemea kuburudisha
wapenzi wa muziki wa dansi kutoka Dar es Salaam leo Ijumaa (31 Januari
2014) katika ukumbi wa Meeda Sinza wilayani Kinondoni.
Akizungumza
kwa niaba ya bendi ya Sikinde, Katibu wa bendi hiyo Hamis Mirambo
amesema “baada ya kukaa muda mrefu bila kufanya shoo yeyote katika
wilaya ya Kinondoni ,bendi ya Sikinde sasa ipo tayari kuwakosha moyo za
wapenzi wa muziki wa dansi katika wilaya hiyo pamoja na watu wa wilaya
za jirani.”
“Tunapenda
kuwaalika wapenzi wote wa muziki wa dansi wasikose kuhudhuria shoo yetu
ambayo itaanza ukumbini Meeda kuanzia saa mbili usiku,” alisema
Mirambo.
Aliongeza,
“Karibuni mpate kuburudika na nyimbo za zamani na mpya kutoka bendi hii
kongwe hapa nchini. Mpate kusikia kutoka kwa msanii Bichuka na wengine
wengi…karibuni sana!”
Kwa
hivi sasa bendi hiyo ya Mlimani Park Orchestra inamalizia kukamilisha
albamu yao mpya iitawayo “Jinamizi la talaka” ambayo inabeba nyimbo kama
Kibogoyo, Deni ntalipa, Ng’ombe haelemewi nunduwe,Kukatika kwa dole gumba, Tabasamu na Mkwezi.
Comments