Mwigizaji, Esha Salim Buheti akiwa hoi kitandani.
MUIGIZAJI aliyelamba tuzo ya Muigizaji Bora wa Kike katika Tamasha la Zanzibar Festival
Film ‘ZIFF’ mwaka huu, Esha Salim Buheti hali yake siyo nzuri na
anahitaji maombi ili apone kutokana na kusumbuliwa na tatizo la uvimbe
kwenye kizazi.Akizungumza na Ijumaa lililokwenda kumjulia hali katika Hospitali ya TMJ iliyopo
Mikocheni jijini Dar, Esha alisema, alifikishwa hospitalini hapo juzi
Jumatano akiwa na hali mbaya kufuatia ‘kuendesha’ ile mbaya. “Nilifikishwa
hapa nikiwa na hali mbaya, nilikuwa ‘naendesha’ sana hadi kufikia hatua
ya kuishiwa nguvu, ilibidi wanichukue vipimo ili kujua tatizo.
Akihudumiwa Hospitalini.
“Baadaye wakaniambia
nina uvimbe kwenye kizazi na UTI, yaani dah! Naomba Mungu anisaidie na
naomba mashabiki wangu pia waniombee nipone,” alisema
Comments