KLABU ya Swansea City imekamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 8 wa Federico Fernandez kutoka Napoli.
Beki
huyo wa kati alikwenda kufanyiwa vipimo vya afya wiki hii Wales na
kusaini Mkataba wa miaka minne, akiweka rekodi ya kuwa mchezaji ghali
zaidi wa nafasi za ulinzi kusajiliwa na klabu za Wales.
Mchezaji
huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye aliichezea Argentina katika Kombe
la Dunia, ataziba pengo la beki wa kati Chico Flores aliyeondoka, kwa
kucheza na Ashley Williams.
Comments