Hebu Tulia na Ujionee Jinsi Maelefu ya Watu Walivyojitokeza Kwenye Tamasha la #Tuo8January Mjini Morogoro



 Msanii wa muziki wa kizazi kipya aitwaye Linah akiimba wimbo wake wa OleThemba,mbele ya mashabiki wake (hawap pichani),waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Tuo8January,lililofanyika kwenye viwanja vya sabasaba jana jioni mjini Morogoro.
  Mmoja wa wasanii mahiri wa Hip hop,ambaye amekuwa akifanya vyema katika anga ya muziki wa kizazi kipya, aitwaye Stamina akitumbuiza mbele ya umati wa wakazi wa mji wa Morogoro katika tamasha la Tuo8January,lenye lengo la kuwahamasisha vijana kujitokeza kushiriki mchakato wa uchaguzi  wa viongozi mbalimbali wanaowataka na wanaowaamini wana uwezo wa kuleta mabadiliko ya kinidhamu kwenye masuala ya msingi ya Taifa letu.
 Msanii mwingine wa hip hop katika anga ya Bongofleva,ambaye amekuwa akifanya vyema kwenye muziki huo,Niki wa Pili akitumbuiza katika jukwaa la wazi la Tuo8Januari lililofanyika mjini Morogoro hapo jana.
 Pichani kati ni msanii Shilole akiwa sambambana madansa wake wakilishambulia jukwaa kwa pamoja mbele ya umati wa wakazi wa mji wa morogoro,waliojitokeza kwenye tamasha la Tuo8Januari,lililofanyika hapo jana katika viwanja vya sabasaba mkoani humo.
  Pichani kulia ni Msanii Mwasiti akiimba wimbo wake wa serebuka akiungwa mkono na shabiki wake kwa kunogesha zaidi jukwaa,huku shangwe za mayowe na vifijo zikiwa zimetawala kutoka kwa mashabiki waliofika katika tamasha la Tuo8January hapo jana.
  Mkali mwingine wa kughani mitindo huru, Godzilla akipanda katika jukwaa la tamasha la Tuo8January,tayari kwa kuwaburudisha wakazi wa mji wa Morogoro waliojitokeza kwa wingi katika tamasha hilo.
 Baadhi ya mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri katika jukwaa la tamasha la Tuo8January,lililofanyika jana katika viwanja vya Sabasaba,mjini Morogoro.
  Baadhi ya wakazi wa mji wa Morogoro wakishangilia yaliyokuwa yakijiri kwenye tamasha la Tuo8January,lililofanyika jana kwenye viwanja vya sabasaba mjini humo,tamasha hilo la wazi ambalo limewashirikisha wasanii mbalimbali,ni kampeni maalum ya kuwahamasisha vijana kushiriki katika chaguzi mbalimbali kwa njia ya matamasha.

Kampeni hiyo ilizinduliwa jijini Dar Desemba 10 mwaka huu na kufanyika tamasha la kwanza mkoani Njombe na sasa Mkoani Morogoro.Baadhi ya Wasanii mbalimbali wenye ushawishi mkubwa kwa vijana wameonesha kuiunga mkono kampeni hiyo, akiwemo Babu Tale, Mwana FA, Nick wa Pili, Lamar, P-Funk, Mwasiti, Barnabas, Ditto, G-nako, Fid Q, Shilole, Yamoto Band, Stamina na wengineo.
  Ilikuwa ni shangwe tu kutoka kwa mashabiki wa muziki wa kizazi kipya kupitia tamasha la Tuo8January
  watazajamaji wakifuatilia kwa umakini yaliyokuwa yakijiri katika jukwaa la Tuo8January hapo jana katika uwanja wa sabasaba mjini Morogoro.
  Sehemu ya umati wa watu waliojitokeza kwenye tamasha hilo la la Tuo8January,lenye lengo la kuwahamasisha vijana kujitokeza kushiriki mchakato wa uchaguzi  wa viongozi mbalimbali wanaowataka na wanaowaamini wana uwezo wa kuleta mabadiliko ya kinidhamu kwenye masuala ya msingi ya Taifa letu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DK NCHIMBI ATINGA MKOANI KATAVI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

NCHIMBI AFUNGUA KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA