ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA NDANI YA CHAKE CHAKE,MKOA WA KUSINI PEMBA LEO.

 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na MNEC wa CCM Taifa,Bwa.Daudi Ismaili pamoja na baadhi ya wanachama wa CCM,mara baada ya kuwasili katika mkutano wa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM,Wilayani Chake  Chake,Mkoa wa Kusini Pembaa mapema leo.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM,Wilayani Chake Chake,Mkoa wa Kusini Pemba mapema leo,ambapo pia Ndugu Kinana alipokea taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi.
 Pichani Kulia ni Mkuu wa Mkoa Kusini Pemba,Mh.Mwanajuma Maggid Abdallah akizungumza jambo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana (pichani shoto),wakati Ndugu Kinana alipokwenda kushiriki ujenzi wa Taifa wa tawi la CCM Mchangani katika jimbo la Wawi,wilaya ya Chake Chake-Mkoa wa Kusini Pemba.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana pichani shoto akishiriki ujenzi wa tawi la CCM Mchangani katika jimbo la Wawi,wilaya ya Chake Chake-Mkoa wa Kusini Pemba akiwa sambamba na Wananchi na wanachama wa CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mbele ya Wananchi wa Uwandani katika jimbo la Wawi,kabla ya kukagua utekelezaji  wa Ilani chama cha Mapinduzi na kushiriki Ujenzi wa Madarasa ya Skuli ya Uwandani
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana sambamba na Wananchi wakishiriki ujenzi wa Madarasa ya Skuli ya Uwandani,katika jimbo la Wawi,wilaya ya Chake Chake,Mkoa Kusini Pemba.Kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa mbele ya katibu Mkuu Ndugu Kinana,imeeleza kuwa mradi wa ujenzi wa jengo hilo litakalokuwa na jumla ya vyumba sita,litagharimu kiasi cha shilingi milioni 18 zitakazomilisha mradi huo.
 Katibu Mkuu wa CCM na ujumbe wake pamoja na wananchi wakikatiza kwenye shamba la miti linalosimamiwa na Kikundi cha Utunzaji Mazingira kiitwacho Hatugombani Cooperative,kilichopo Kilindi,Wilaya ya Chake Chake,mkoa wa Kusini Pemba.Kikundi hicho kina jumla ya Wanachama wapatao 49,ambapo shughuli kubwa ya kikudi hicho ni utunzaji wa mazingira kwa upandaji miti ya Mivinje,Mikaratusi,Mikungu na Mitondoo.Mradi huo wa kuhifadhi Mazingira una eneo la eka 20,ambapo mpaka sasa mradi huo una thamani ya shilingi Milioni 40 na zaidi
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akishiriki kupanda mti katika shamba la miti linalosimamiwa na Kikundi cha Utunzaji Mazingira kiitwacho Hatugombani Cooperative,kilichopo Kilindi,Wilaya ya Chake Chake,mkoa wa Kusini Pemba.Kikundi hicho kina jumla ya Wanachama wapatao 49,ambapo shughuli kubwa ya kikudi hicho ni utunzaji wa mazingira kwa upandaji miti ya Mivinje,Mikaratusi,Mikungu na Mitondoo.Mradi huo wa kuhifadhi Mazingira una eneo la eka 20,ambapo mpaka sasa mradi huo una thamani ya shilingi Milioni 40 na zaidi
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akielekea katika kijiji cha Chanjamjawiri,jimbo la Chake Chake akiwa ameongoza na viongozi mbalimbali wa CCM Wilaya na Mkoa CCM Kusini Pemba kushiriki upandaji wa miche ya Mikarafu,katika ushirika wa uitwao Hatukosani wenye jumla ya Watu 25.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishiriki kuotesha miche ya Mikarafuu katika bustani ya kikunndi cha Hatukosani,wakati alipotembelea na kukagua shughuli zinazofanywa na kikundi hicho chenye wanachama wapatao 25 kilichopo Chanjamjawiri-Chake Chake mkoa wa Kusini Pemba.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipewa taarifa ya kikundi cha Ushirika cha Jitihada Mbele cha Ufugaji  wa Samaki chenye jumla ya wanachama 10.Kikundi hicho kilianzishwa kwa lengo la Ufugaji wa samaki ili waweze kujikwamua kiuchumi na pia kusimamia sera ya chama cha CCM,ikiwemo kujikusanya kwa pamoja ili kuanzisha vikundi vya ushirika kwa ajili ya kujiajiri wenyewe.Kwa Mujibu wa Msomaji wa taarifa alieleza kuwa mradi huo wa samaki una jumla ya thamani ya shilingi milioni 10.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishirik kuchimba moja ya mabwawa ya wanakikundi hao wa Jitihada Mbele akiwa sambamba na baadhi ya wananchi na wanachama wa CCM. 
 Mbunge wa Viti Maalum Pemba,Mh.Faida Bakari akifafanua mambo mbalimbali yaliyomo ndani ya Katiba mpya inayopendekezwa,inayotarajiwa kupigiwa kura mnamo Aprili 30,Mbunge huyo ameawata Wananchi wa Pemba kuipigia kura ya ndio katiba hiyo ili ipite,kwani ina mambo mengi mazuri kwa Zanzibar
 Baadhi ya Wanachi wakifuatilia kwa makini mkutano wa hadhara uliofanyika mapema jioni ya leo Pujini Kunvini Chake Chake mkoa wa Kusini Pemba.
Mbunge wa Viti Maalum,Mh.Asha Abdul Haji akihutubia katika mkutano wa hadhara  uliofanyika mapema jioni ya leo Pujini Kunvini Chake Chake mkoa wa Kusini Pemba,ambapo pia Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana aliwahutubia wananchi wa eneo hilo.
Baadhi ya Wanachama wa CCM wakishangilia jambo katika mkutanno wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Pujin Kumvini-Chake Chake mkoa wa Kusini Pemba. 
 Mfuasi wa Chama cha CUF Ghalib Bedui Khamis akikabidhi kadi yake kwa katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na kukabidhiwa kadi mpya ya uanachama wa CCM.
 Mfuasi wa Chama cha CUF Said Abdallah Ibrahim akionesha kadi yake ya zamani kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kabla ya kukabidhi na kupewa kadi mpya ya uanachama wa CCM,mbele ya Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Pujini Kunvini Chake Chake mkoa wa Kusini Pemba.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo kwenye uwanja wa Pujini Chake Chake,mkoa wa Kusini Unguja

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA