MBUNGE MH. JOSHUA NASARI AONGOZA MAZISHI YA ALIYEKUWA MWANAFUNZI WA IFM EMMANUEL P. PALLANGYO ,SING'ISI MERU ARUSHA.

 

Mbunge wa Arumeru Mashariki Mh. Joshua Nasary akitoa salamu za Pole kwa wafiwa wote wakati wa mazishi ya Marehemu Emmanuel Pendael Pallangyo aliyefariki Tarehe 7.02.2015 na kuzikwa kijijini kwao Sing'isi Meru tarehe 12.02.2015 .
Baba wa Marehemu Mzee Pendael T.  Pallangyo akitoa Salam zake za Mwisho kwa Mwanae Mpendwa Emmanuel Pallangyo
Kaka Mkubwa wa Marehemu Elisante Pallangyo, akifuatiwa na Dada zake Eliakunda  Pallangyo, Magreth Pallangyo pamoja na Sarah Pallangyo wakitoa Heshima za Mwisho  katika Mwili wa Marehemu Emmanuel Pendael Pallangyo Kijijini kwao Sing'isi Meru  Arusha.
Wa kwanza kulia ni Mbunge wa Arumeru Mashariki Mh.  Joshua Nasary akiwa na kwenye msiba wa Marehemu Emmanuel Pallangyo ambaye alikuwa ni Mwanafunzi wa IFM nyumbani kwao Sing'isi Meru.
Mmoja wa wanafamilia akisoma Wasifu wa Marehemu Emannuel Pendael Pallangyo
Msaidizi wa Askofu mkuu wa Jimbo la Kaskazini   Paulo Urio akiongoza Ibada ya Mazishi ya Marehemu Emmanuel Pendael Pallangyo kijijini kwao Sing'isi Meru.
Baadhi ya viongozi wa Dini kutoka Madhehebu Mbalimbali wakiwa wanaimba na waombolezaji wengine wakati wa ibada ya  Mazishi.
Mkuu wa jimbo la KKT kaskazini  Zelote Pallangyo akitoa Mahubiri wakati wa Misa ya mazishi ya Marehemu Emmanuel Pallangyo kijijini kwao Sing'isi Meru.
 Aliyeteuliwa kuzungumza kwa niaba ya Familia Bwana Exaud Assery Pallangyo akitoa salamu za shukurani za pekee kwa watu wote waliohudhuria Mazishi ya Mpendwa wao Emmanuel Pendael Pallangyo aliyefariki Tarehe 7.02.2015 Jijini Dar es salaam na kuzikwa Tarehe 12.02.2015 Nyumbani kwao Sing'isi Meru.
Baadhi ya ndugu wa Marehemu Emmanuel Pendael Pallangyo aliyefariki tarehe 7.02.2015 wakiwa na simanzi wakati wa Ibada ya Mazishi kijijini kwao Sing'isi Meru
Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika Ibada ya Mazishi ya Marehemu Emmanuel Pallangyo kijijini kwao Sing'isi Meru.
Mwili wa Marehemu Emmanuel Pendael Pallangyo ukipelekwa Makaburini kijijini kwao Sing'isi Meru kwa ajili ya Mazishi.
Baba wa Marehemu Mzee Pendael T.  Pallangyo kushoto akiweka Shada la maua katika Kaburi la Mwanae Emmanuel Pendael Pallangyo.
Mh. Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nasary akiweka Shada la maua katika Kaburi la Marehemu Emmanuel Pendael Pallangyo aliyefariki Tarehe 7.02.2015 na kuzikwa tarehe 12.02.2015 kijijini kwao Sing'isi Meru
Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Jimbo la Kaskazini   Paulo Urio akimaliza Ibada Makaburini kwa kutoa Mbaraka kwa watu wote waliofika katika mazishi ya Marehemu Emmanuel Pendael Pallangyo yaliyofanyikia kijijini kwao Sing'isi Meru.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa Makaburini wakati wa mazishi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.