SERIKALI YATANGAZA RASMI KUWATAMBUA MABLOGA NCHINI


 Mwanachama wa Chama cha Mabloga Tanzania (TBN), Krantz Mwantebele akifafanua jambo alipokuwa akitoa somo kuhusu njia 10 za kumuwezesha bloga kuingiza kupata fedha kupitia kwenye blog wakati wa Mkutano Mkuu wa chama hicho Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Hassan Abbas akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa  wanachama wa TBN, Dar es Salaam jana, ambapo alisema kuwa Serikali inatambua mabloga Tanzania, na kwamba wako tayari kufanya nao kazi za kujenga nchi.
 Mwenyekiti wa Muda wa TBN, Joachim Mushi akitoa neno kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Habari -Maelezo, Hassan Abbas  (wa pili kulia) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Muda wa chama hicho, Khadija Kalili na Kulia ni Kaimu Meneja Mwandamizi Amana, Huduma za Bima na Huduma za Ziada wa Benki ya NMB, Stephen Adili. NMB ndiyo wadhamini wakuu wa mkutano huo. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA)

 Baadhi ya wanachama wa TBN wakisikiliza kwa makini wakati wa mkutano huo mkuu
 Mmiliki wa Michuzi Blog, Muhidini Issa Michuzi akichangia hoja wakati wa mkutano huo. Kushoto ni Mmiliki wa Blog ya Wananchi,  William Malecela.
 Mwenyekiti wa Muda wa TBN, Joachim Mushi akiwa na Mkurugenzi wa MAELEZO, Hassan Abbas
 William Malecela, Le Mutuz akichangia mada wakati wa mkutano huo.
 Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog akiuliza swali wakati wa mkutano huo.
 Bloga John Kitime akichangia mada wakati wa mkutano huo
 Kaimu Meneja Mwandamizi Amana, Huduma za Bima na Huduma za Ziada wa Benki ya NMB, Stephen Adili akielezea kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo.
 Meneja wa Mo Blog (kulia), akijaza fomu kujiunga na Benki ya NMB kwa huduma ya kupata kadi ya Chap Chap. Katikati ni Ofisa Mauzo wa NMB, Evance Shirima na Katibu Mkuu wa Muda wa TBN, Khadija Kalili.
Mkurugenzi wa MAELEZO, Hassan Abbas (katikati) akijibu maswali mbalimbali ya wanachama wa TBN

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA