KWA HERI KAMANDA WETU ABBAS KANDORO

KWAHERI!! MTWA Cadre Baba Mhe Ndugu Comrade Abbas Kandoro "MWAGITO"; MUNGU AKULAZE MAHALA PEMA PEPONI MYALUKOLO; Tulikuzoea, Tulikupenda, Tuliwiwa na Upendo wako wa dhati katika Kujenga Maisha yetu Kisiasa, Kiuchumi na hata Kijamii; Uliongea kwa Taratibu iliyojaa Tunu ya Busara, Hekima na Upendo!! MTWA Baba Mhe Abbas Kandoro ulichukua Kijiti cha Kulijenga Jiji la Arusha Mwaka, 2006 kutoka kwa Mhe Mohammed Babu, na bado Ukatumikia Utumishi wako kwa Kumpa Kijiti Mhe Samuel Ndomba; Hilo ni Jiji uliliongoza kwa Umahiri Mkubwa Ustahdhi Abbas Kandoro; Ni Mkuu wa Mkoa pekee wa Jiji la Dar-es-salaam aliyeweka heshima kwa Wauzaji wadogowadogo “Matching-guy” katika Mtaa wa Condo na Mitaa mingine katika Jiji la Dar-es-salaam “the house of peace" yaani “Nyumba ya Amani”; Jiji ambalo zamani liliitwa Mzizima; Jiji lililokana katukatu kuitwa "house of war" (Dar al-harb) yaani ‘Nyumba ya Vita”; Sitosahau ulipounda Tume ya Uchunguzi kuchunguza Chanzo cha Kuanguka kwa Jengo lenye ghorofa Kumi hapa jijini lililoanguka Jumamosi ya Tarehe 21 Juni, 2008 alfajiri na kuuwa watu wanne na kujeruhi watu kadhaa na huku mwili wa mtu mmoja ukifukuliwa akiwa amekufa kutoka katika kifusi cha Jengo hilo; Uliwaamini Wajumbe wazito uliowateua akina Mhandisi Joseph Malango kutoka Bodi ya Wakandarasi, Eng(Arch)Elias Mwakalinga kutoka Wizara ya Miundombinu, Luteni Kanali Mkohi Kichogo kutoka Jeshi la Wananchi Wa Tanzania, Mhandisi Dkt Kiguma kutoka Usalama wa Taifa, Ndugu Daniel Mtupa kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB), Ndugu Joseph Ringo kutoka Bodi ya Usanifu wa Majengo, Dkt Paul Ndumbalo kutoka Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam; Hawa wote hakika ni Vichwa vya Uhakika, Hayati wetu wewe!! Hatimaye ukamwachia Jiji hili Mhe William Vangimembe Lukuvi; Utawambia nini Wakazi wa Mwanza, “The Rock City” walivyofaidi Bidii zako za kulifanya Jiji la Mfano Mzee Kandoro wewe!! Ukabeba Majukumu Kuanzia Mwaka, 2009 hadi Mwaka, 2011; Jiji la Mwanza likitamkwa huwezi kuacha kuoanisha na Jina lako Tukufu la Abass Kandoro!!; Ukilichukua Jiji hilo kutoka kwa Mhe Eng Dkt James Msekela na Kumuachia Kijiti Mhe Eng Evarist Ndikilo; Ulichukua kwa Mhandisi ukamwachia Mhandisi, siri anayo Mhe Ndugu Dkt Col Jakaya Halfani Mrisho Kikwete; Kabla ya kupelekwa Mbeya niliipata habari kuwa unaondoka Mwanza; Mimi Handley Mtoto wa Stella!! Sikujua Unaenda Kwetu Mbeya “The Scoland of Africa”, “The Green-City”; Nikakupigia Simu; Mzee naomba Uje kwenye Chama usaidie Dawati la Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi!! Ukanijibu bila Kusita “Mafwenga!! I am not interested to serve in the Party as active politician in advocacy desk, but let me think on your advice”: Mara Ukapelekwa Nyumbani Mbeya………………………….Duu MTWA Comrade Abass Kandoro Umeniliza Mtani wangu: Kwa kweli, sitosahau Ulipolisimamia Jiji la Mbeya, mara Ulipoteuliwa Tarehe 16 Septemba, 2011 na Kuapishwa saa 4.00 Asubuhi katika Viwanja vya Ikulu, kwani moja ya Kitu kilichonigusa ni pale ulipofanya mkutano wa hadhara saa 11.00 alfajiri, katika kituo kikuu cha mabasi Jijini Mbeya uliowahusisha abiria na madereva wa mabasi makubwa; Ulikuwa Mtatuzi wa Kero, Mtatuzi wa Migogoro Mhe Kandoro; Ulitatua Vifo vya ajali hasa pale ulipotoa Takwimu ukisema tangu Januari hadi Tarehe 14/09/2014, kuwa ajali 297 zilitokea na kusababisha vifo vya watu 210 na majeruhi 402; Kwa lugha ya aina yake ya Upole na Ukali wenye Diplomasia ya Kubembeleza ukasema “Madereva, chonde chonde kuweni makini mnapokuwa kwenye usukani, endesheni kwa kufuata sheria na taratibu ili kupunguza ajali zisizo za lazima’’; Sitosahau Program yako ya kutusaidia Tuuze Mazao yetu Dubai, Sisi wana Mbeya! Sisi! sisi! Tulioziea zaidi Biashara ya Ndizi na Mchele; Uliweka kivutio cha Maksudi ukisisitiza umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Songwe!! KIKI BE!! KIKI MWAGITO!! KIKI MTWA? HAYA BWANA!! Aidha, uliwafundisha Mbeya kuheshimu na Kutunza Mazingira ukiwataka Viongozi wa Jiji hilo kuingilia kati kunusuru hali ya uchafu iliyokithiri ndani ya jiji la Mbeya kwa kuwataka Viongozi kusimamia Sheria; Ulipambana na Wizi wa Kutumia Mitandao na hukusita kuwasiliana na Mamlaka ya Mawasilino Tanzania (TCRA) kushirikiana na kampuni za simu za mkononi kudhibiti wimbi la wizi wa Kutumia Mitandao, Baba Ulienda sambamba na Techological changes!!; Hakika ulirinusuru Jiji hilo kuitwa “shamba la bibi,”; Aidha, Hukusita Mnamo Tarehe 17 Machi 2016 Ulipomkabidhi Majukumu Mazito ya Mkowa wa Mbeya Comrade Amosi Makala; Hakika "Medali ya Utumishi Uliotukuka" Uliotuzwa na Mhe Ndugu Dkt Col Jakaya Mrisho Halfani Kikwete imetuachia alama kubwa ya Utumishi na Utawala Bora hapa Nchini; Utawambia nini Wakazi wa Singida leo jinsi ulivyowatumikia? Wasalimie Mtwa Mkwawa! Mtwa Amran Mayagila! Mtwa Peter Mgongolwa Siyovelwa! na wengine wengi waliotangulia Mbeleza za Haki: "Inna lillaahi wa inna ilayhi Raaji'oon" MTWA CADRE NDUGU MHE COMRADE ABASS KANDORO (Prof (Dr) Comrade Handley Mpoki Mafwenga Simba Mwai-Holler Nkulu Gwa Kipanga “MUNDU GWA JESU”)
LikeShow more reactions
Comment

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA