WASOMI WA CHUO KIKUU DODOMA KUJITOLEA KUFUNDISHA SEKONDARI MUSOMA VIJIJINI


 

Jimbo la Musoma Vijijini lina Sekondari 22 za Kata/Serikali na 2 za Binafsi.


Upungufu wa Walimu ni mkubwa sana. Serikali inajitahidi kutoa ajira mpya na bado upungufu ni mkubwa.


WALIMU WA KUJITOLEA

Vijana wetu wanaosoma UDOM wako tayari kujitolea kufundisha kuanzia mwezi ujao, Julai 2022.


OMBI hilo limefikishwa kwa Mbunge wa Jimbo.


OMBI LA UPATIKANAJI WA POSHO ZA WALIMU WA KUJITOLEA


WAZALIWA au wenye chimbuko la Jimboni mwetu wanaombwa WAJITOKEZE kuchangia POSHO za hao vijana wetu waliotayari kufundisha kwa kujitolea.


Kiwango cha posho hizo, kwa ujumla wake ni kati ya Tshs 200,000 na 400,000 kwa mwezi. Makubaliano yatafanywa kati ya Uongozi wa Sekondari husika na Mwanafunzi anayejitolea.


Tunaomba walioko tayari kuchangia posho hizo wajitokeze.


Mchangiaji anaweza kuchagua Sekondari anayopenda kuchangia na Ofisi ya Mbunge itamuunganisha na chaguo lake. 


Orodha ya WACHANGIAJI ikipatikana VIONGOZI wa  Wanafunzi hao (UDOM) watapewa taarifa.


Waliokuwa tayari kuchangia wawasiliane moja kwa moja na Mbunge wa Jimbo

Namba:

+255 754 400 800


Wengine wanaweza kuwasiliana moja kwa moja na Sekondari wanazopenda kuzichangia.


Ofisi ya Mbunge

Jimbo la Musoma Vijijini

www.musomavijijini.or.tz


Tarehe:

Jumamosi, 11.6.2022



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

KWA KHERI MAKARANGA UMEUTIMIZA MWENDO...

KATI YA WATOTO 7 WA HAYATI MAGUFULI ANAYEJULIKANA ZAIDI NI JESCA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

KIKOSI KILICHOITWA TAIFA STARS HIKI HAPA

UBORA UNAONEKANA: BENKI YA NMB YANG'ARA TUZO ZA EUROMONEY 2026

KIJANA WA KINYAKYUSA WA ENZI HIZO, NUSURA AMCHAPE WAZIRI MUONGO BUNGENI

WANAJESHI WAGOMA KWENDA IRAN KUPIGA