Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amethibitisha kifo cha Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro Tixon Nzunda kilichotokea kwa ajali ya gari, ambapo amesema "ajali hiyo imetokea muda wa saa nane kuelekea saa tisa mchana leo, Juni 18, 2024".
"Ni kweli wakati anatoka KIA amepata ajali mbaya sana, ndio na mimi nakwenda eneo la ajali,"-amesema RC Babu
Aidha pia Dereva wa Katibu Tawala huyo Alphonce Edson amefariki Dunia katika ajali hiyo.
Babu amebainisha kuwa muda mfupi kabla ya ajali hiyo, Marehemu Nzunda alikuwa na kikao na wadau wa maendeleo kutoka nchini Namibia kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.
Comments