ORGANIC MORINGA YATOA RAI KWA JAMII KUTUMIA BIDHAA ZA MLONGE

 


NA MWANDISHI WETU


KAMPUNI ya Organic Moringa Limited, imeitoa rai kwa jamii kutumia bidhaa zinazitokana na Mlonge kwa kuwa zina virutubisho vingi.


Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Organic Moringa, Sebastian Msapalla wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni jijini Dodoma


"Jamaii imeendelea kuzalisha bidhaa mbalimbali za asili kwa kutumia mimea yenye virutubisho, ikiwemo mlonge, uwi, rosela, mbegu za chia, mchele wa kahawia pamoja na asali inayozalishwa katika mazingira yenye miti ya mlonge," amesema.


Amesema kampuni hiyo inalenga kuwapatia wananchi bidhaa zinazotokana na maliasili na zinazoweza kutumika kama sehemu ya lishe yenye virutubisho.


Miongoni mwa bidhaa zinazotolewa na kampuni hiyo ni unga wa majani ya mlonge, ambao hutengenezwa kwa kuzingatia taratibu za usindikaji ili kuhifadhi virutubisho vinavyopatikana kwenye majani ya mlonge. 


Msapalla amesema, bidhaa hiyo imeandaliwa kwa matumizi ya binadamu na inaweza kutumika kuongeza virutubisho katika lishe.


Aidha, Organic Moringa imekuja na bidhaa nyingine inayojulikana kama Moringa Root Powder, ambayo ni unga unaotokana na mzizi wa mlonge. Kampuni inaeleza kuwa bidhaa hiyo hutumika katika tiba asili, huku ikisisitiza umuhimu wa matumizi sahihi na kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

Soma Taarifa ya UTEUZI:Rais Jakaya Kikwete amemteua Dkt. Ben E. Moshi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya PUMA Energy (zamani ilijulikana kama BP Ltd)

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

OWM–TAMISEMI YASHINDA TUZO YA MABADILIKO YA KIDIJITALI KATIKA TEHAMA AWARDS 2026

BINTI WA KITANZANIA GLORIA MAJULE ASHINDA TUZO YA UANDISHI BORA WA FILAMU YA MALARIA MAREKANI ‎

KOCHA WA MC ALGERS AIHOFIA YANGA

VIONGOZI NA WATENDAJI WA MATAWI UVCCM PANGANI WANOLEWA

MAMBO 16 USIYOYAJUA KUHUSU RAIS MSTAAFU DKT. JAKAYA KIKWETE

HIZI HAPA TAKWIMU ZA PETER SHALULILE MCHEZAJI MPYA WA YANGA SC 🔰 🔥