WIZARA YA ELIMU YAWAALIKA WANAFUNZI WA VYUO KUSHIRIKI UTOAJI MAONI MABADILIKO YA MITAALA YA ELIMU

 

 Mkurugenzi wa Elimu ya Juu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Hosea Kennedy amewaalika wanafunzi wanachama wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo na Vyuo Vikuu (TAHLISO) kushiriki katika makongamano ya kutoa maoni kuhusu mabadiliko ya sera na mitaala ya elimu.

Aidha amewataka vijana hao kushiriki vyema kutoa elimu juu ya umuhimu wa sensa katika maeneo yao. Kennedy ameyasema hayo wakati wa Kongamano lililoandaliwa na TAHLISO kuhusu umuhimu wa Sensa kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma Mei 21, 2022. Kongamano hilo lilihudhuriwa pia na Kamisaa wa Sensa, Spika mstaafu, Anne Makinda.

Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video, Kennedy akizungumza katika mkutano huo....
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MSIMAMIZI MKUU
KAMANDA WA MATUKIO TV/BLOG
0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MASIKINI

MAKUNDI YA VILABU VINAVYOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2025.

JINSI YA KUMTAWALA MWANAMKE HASA MKE (USIOE MKE WA MTU)

MUONEKANO WA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA MSALATO

DIARRA KIPA BORA TANZANIA

CHINYELE ACHUKUA FOMU KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE DODOMA MJINI