Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango leo anawaongoza Watanzania katika maombi na dua maalum ya kuliombea taifa katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Picha baadhi ya viongozi wa Serikali na Dini wakiwa katika shamrashamra hizo zinazoendelea katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Ikumbukwe kuwa mwaka huu April 26 Tanzania inaadhimisha miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sherehe hizo zitafanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam na Mgeni rasmi ni Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan
(Imeandikwa na Manase Madelemu)
Comments