RAIS WA JAMHURI YA SOMALIA MHE. HASSAN MOHAHADAIPONGEZA TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE (JKCI)

  Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud akisaini kitabu cha wageni Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mara alipoitembelea Taasisi hiyo kujionea mtambo wa Cathlab ambao ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya moyo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Moyo na Dkt. Bingwa Magonjwa ya Moyo Dkt. Peter Kisenge.

   Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Moyo na Dkt. Bingwa Magonjwa ya Moyo Dkt. Peter Kisenge. mara alipoitembelea Taasisi hiyo kujionea mtambo wa Cathlab ambao ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya moyo. Wa katikati anae shuhudia ni Waziri wa Afya Nchini Tanzania Mhe. Ummy Mwalimu.
  Waziri wa Afya  Nchini Tanzania Ummy Mwalimu akizungumza katika chumba cha Cathlab na Mhe Rais wa Jamuhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud jinsi mtambo unavyo fanya kazi.
  Rais wa Jamuhuri ya Somali akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo ya Jalaya Kikwete mara baada ya kuitembele na kujionea mtambo wa Cathlab ambao ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya moyo. 

  Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akiwapungia mkono Viongozi na Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mara baada ya kujionea mtambo wa Cathlab ambao ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu  ya moyo. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
 

Na Mwandishi Maalumu -  Dar es Salaam


27/4/2024 Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud amewapongeza wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa huduma nzuri wanayoitoa ya kuokoa maisha ya watu wenye matatizo ya moyo.


Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud  alizitoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam alipotembelea Taasisi hiyo  (JKCI) kwaajili ya kuona  huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.


Akiwa katika Taasisi hiyo Mhe. Rais Mahamud alitembelea maeneo mbalimbali  ya JKCI ikiwa ni pamoja na mtambo wa Cathlab ambayo ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu  ya moyo.


Akizungumzia kuhusu ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema JKCI ni moja ya Taasisi inayoongoza katika nchi za Afrika Mashariki na kati katika kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo.


Dkt. Kisenge alisema Rais Mohamud alitembelea Taasisi hiyo kwaajili ya  kuona namna ambavyo nchi ya Somalia itawapeleka wagonjwa wa moyo JKCI kupata  tiba ya matibabu ya moyo.


“Nchi ya Somalia inawapeleka wagonjwa wengi  wa moyo kwenda kutibiwa katika nchi za India, Ulaya na Marekani  wakati huduma hii inapatikana nchini Tanzania, na ukiangalia nchi hizi ziko karibu hivyo basi itakuwa ni rahisi kwao kuwaleta wagonjwa kuja kutibiwa hapa kwetu”.


“Kuja kwa wagonjwa hawa kutaisaidia nchi yetu kukua kiuchumi kwani pesa zitakazopatikana zitawafikia watu wengi ikiwemo wamiliki wa hoteli ambako wagonjwa watalala pamoja na wafanyabiashara watakaowauzia vyakula na mahitaji mengine”, alisema Dkt. Kisenge.


 Dkt. Kisenge alimshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuzidi kuimarisha mahusiano na nchi za nje ndiyo maana watu wengi wanakuja kuwekeza hapa nchi hata Taasisi hiyo imekuwa ikiwapokea  wageni mbalimbali kutoka nchi za nje.


Akiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud pamoja na ujumbe wake aliambata na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MUSTAFA MKULO AFARIKI DUNIA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

YANGA BADO POINTI 2 TU ITANGAZE UBINGWA

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

MAKALLA ASHANGILIWA BUNGENI

BASHASHA LATAWALA NCHIMBI ALIPOLAKIWA NA CHONGOLO SONGWE

DKT NCHIMBI AKARIBISHWA KIMILA NYUMBANI RUVUMA

DKT NCHIMBI AZURU KABURI LA JOHN KOMBA LITUHI, NYASA