Ukubwa wa Jimbo la Musoma Vijijini
Kata 21 zenye vijiji 68 na vitongoji 374
Idadi ya Shule za Sekondari
Sekondari za Kata/Serikali: 26
Sekondari za Binafsi: 2
Sekondari mpya zinazojengwa: 12
Idadi ya Maabara za Masomo ya Sayansi (physics, chemistry & biology) kwenye Sekondari za Kata
Maabara zinazohitajika: 78
Maabara zilizopo: 41
(i) Sekondari 7: zina maabara tatu
(ii) Sekondari 8: zina maabara mbili
(iii) Sekondari 4: zina maabara moja
(iv) Sekondari 7: hazina maabara
Kampeni ya ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi
Wananchi na viongozi wao wanashirikiana na Serikali kuharakisha ujenzi wa maabara tatu kwenye kila Sekondari ya Kata.
Ujenzi unaendelea na Mbunge wa Jimbo anaendelea kupiga Harambee za ujenzi huu.
(i) Sekondari ambazo hazina maabara ni:
Bukwaya, Busambara, Mtiro, Murangi, Nyanja, Seka na Tegeruka
(ii) Sekondari zenye maabara moja ni:
Bukima, Dan Mapigano, Kasoma na Mabuimerafuru
WITO WA KUCHANGIA
Wadau wa Maendeleo na hasa Wazaliwa wa Musoma Vijijini wanaombwa wajitokeze kuchangia ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi kwenye Sekondari zetu za Kata.
Picha zilizoambatanishwa hapa zinaonesha:
Baadhi ya maabara zilizojengwa kwa ushirikiano mzuri wa wanavijiji, viongozi wao na Serikali yetu.
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
Tarehe:
Jumapili, 6.10.2024
Comments