NYERERE ALIVYOIKEMEA MAREKANI BAADA YA KUDONDOSHA MABOMU IKULU YA LIBYA

 


'Wakati Afrika imejitahidi kutokomeza Ukoloni wa Smith kule Rhodesia mimi ninayoijua kama Zimbabwe ,OAU inakabiliwa tena na changamoto kubwa na kongwe ya Ubeberu wa nchi za Magharibi.Ni bahati mbaya sana sana hili linatugawa hata ndani ya OAU.

Sisemi na sitathubutu kusema tuko wamoja kwenye hili na tuna nia thabiti ya kutokomeza ubeberu wa Magharibi dhidi ya Afrika hii ni kwasababu wako watu humo humo ndani si wenzetu katika safari hii ngumu,ila tukiamua tunaweza.

Kama kwa pamoja sisi OAU tumeweza kumkemea na kumlaani Kaburu kwa kuendesha serikali ya Kibaguzi ndivyo hivyo tuiambie Marekani na vibaraka wake wasiwe Polisi wa Dunia katika kuhukumu kila jambo na hili hatuhitaji kwenda UNO hili tutalikemea popote pale bila kuoneana aibu"

Kauli ya Dr Julius Kambarage Nyerere akiongea na BBC nyumbani kwake Msasani Jijini Dar es Salaam baada ya ndege za kijeshi za Marekani kushambulia Ikulu ya Rais wa Libya Kanali Muamar Ghaddaf na kumuua mtoto wa kurithi wa Rais huyo.

Shambulio hilo linaelezwa kuwa lilikuwa ni la kulipiza kisasi baada ya ndege ya abiria ya Marekani ya Shirika la PAN AM ikiwa na abiria 198 kuangushwa katika anga la Lockbie Scotland kwa bomu lililotegwa katika redio ndogo mwaka1989.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

𝗠𝗕𝗢𝗪𝗘 𝗔𝗦𝗜𝗧𝗜𝗦𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗡𝗗𝗔𝗠𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗖𝗛𝗔𝗗𝗘𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗧𝗔𝗥𝗘𝗛𝗘 𝟮𝟯.

USHAURI WA BURE KWA KILA MFANYAKAZI

KIKOSI CHA CBE KIMEWASILI ZENJI KUVAANA NA YANGA

TAKUKURU YAPONGEZWA KUWA BEGA KWA BEGA NA MBIO ZA SEPESHA ZINAZOPINGA RUSHWA YA NGONO

NDOGO WA MUME WANGU ALIKUWA EX WANGU