WAZIRI CHANA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA MRADI WA REGROW KIHESA KILOLO

 Na Happiness Shayo - Iringa 

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amefanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa kituo cha utalii cha Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na kituo cha utafiti cha Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) inayotekelezwa chini ya mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW), Kihesa Kilolo Mkoani Iringa.


Mhe. Chana amejionea maendeleo ya mradi huo ambapo mradi wa ujenzi wa kituo cha utalii wenye thamani ya shilingi bilioni 21.4 umefikia asilimia 31 na kituo cha utafiti chenye thamani ya shilingi bilioni 1.55 kimefikia asilimia 80.


Ikumbukwe kuwa mnamo Septemba 7, 2024 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ilifanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi hiyo na kuelekeza Wakandarasi kusimamia mikataba yao na kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.


Mhe. Chana yuko Mkoani Iringa kwa ziara ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.


Dk. Chana akikagua maendeleo ya ujenzi wa kituo cha utafiti cha Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI). 


Waziri Dk. Chana akikagua ujenzi wa jengo la Kituo cha Utalii cha Bodi ya Utalii (TTB).


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

OWM–TAMISEMI YASHINDA TUZO YA MABADILIKO YA KIDIJITALI KATIKA TEHAMA AWARDS 2026

MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA KUAPISHWA NDEJEMBI KUWA MAKAMU WA RAIS

NI MAKOSA WANAFUNZI KUFIKA SHULE SAA 1:15 ASUBUHI

MAFAO YA MAKAMU WA RAIS ALIYEJIUZULU

URUSI, CHINA, IRANI NA KOREA KASKAZINI WAPANGA KUUNDA JESHI MOJA LA KUJIHAMI

NDEJEMBI KUTOKA MFANYAKAZI WA GSM HADI KUWA MAKAMU WA RAIS