KARIBUNI TUCHANGIE UJENZI WA SEKONDARI MPYA KUMI NA MBILI (12) MUSOMA VIJIJINI


 

*Kumbukumbu:*

Naomba kuwakumbusha kwamba hivi karibuni Mbunge wa Jimbo aligawa Saruji Mifuko 150 kwa kila kijiji kinachojenga sekondari mpya. Fedha za saruji hiyo ni zile za Mfuko wa Jimbo


Kijiji cha Mmahare, Kata ya Etaro kinaenda kwa kasi nzuri na tayari kimetumia mifuko yote 150 - hongereni!


*HARAMBEE za Mbunge wa Jimbo:*


Kwenye miradi yote ya ujenzi ya Jimboni mwetu, Mbunge wa Jimbo huwa anapiga HARAMBEE kuchangia ujenzi unaofanywa kwa kutumia nguvukazi na michango ya fedha za wanavijiji.


*HARAMBEE ya Kijiji cha Mmahare:*


Wanakijiji: Saruji Mifuko 155

Mbunge wa Jimbo: Saruji Mifuko 155


Saruji Mifuko 50:

Leo, Mbunge wa Jimbo ameipatia Kamati ya Ujenzi ya Mmahare Sekondari saruji hiyo, yaani mifuko 50 kati ya 155. Wakiimaliza ipasavyo, wanaongezewa. 


 *Picha iliyoambatanishwa hapa inaonesha:*


Ujenzi wa msingi wa kwanza wa majengo ya Mmahare Sekondari ya Kijiji cha Mmahare, Kata ya Etaro. Ujenzi wa umsingi huo utakamilishwa leo, 10.3.2025


Hii ni sekondari ya tatu ya Kata ya Etaro!




Ofisi ya Mbunge 

Jimbo la Musoma Vijijini 

www.musomavijijini.or.tz 


P. O. Box 6

Musoma 


Tarehe:

Jumatatu, 10 Machi 2025

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

RAIS TRUMP ARARUANA NA RAIS WA UKRAINE

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

SERIKALI YALIKUBALI OMBI LA DIAMOND

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

ARAJIGA AULA KOMBE LA DUNIA