HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO



Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Imeanzisha matibabu ya kuziba mapengo  
Vipandikizi Meno (Dental Implant), ambapo mzizi bandia hupandikizwa kwenye taya, kisha kuwekewa meno juu yake yanayogandishwa na kutumika kama sehemu ya meno yake ya kuzaliwa nayo.


Aidha, Serikali imewezesha hospitali hiyo kununua mashine ya kisasa kabisa inayowezesha uchunguzi wa magonjwa ya mifupa ya taya pamoja na CT scan ya uso na kichwa kusaidia kupanga upandikizaji wa vipandikizi vya meno ambapo tangu kununuliwa mwishoni mwa mwaka 2024 tayari wagonjwa 2,251 wamenufaika.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Huduma ya Upasuaji wa hospitali hiyo, Dkt. Rachel Mhaville alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  katika Ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma Machi 6, 2025, kuhusu mafanikio ya MNH katika miaka minne ya ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.


Dkt. Mhaville ambaye kwenye mkutano huo alikuwa anazungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa MNH, Prof. Mohamed Janabi, amesema kuwa wameanzisha huduma nyingine ya kuondoa sehemu yenye ugonjwa kwenye taya kisha kuvuna sehemu ya mbavu pamoja na mfupa wa nyonga kwa kutumia vipandikizi maalum kuunda mfupa wa taya jipya la chini ili kumrejeshea mgonjwa muonekano mzuri lakini pia huweza kupandikizwa meno na kumrejeshea mgonjwa uwezo wa kula tena.


Dkt. Mhavile akizungumza katika mkutano huo.
Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.


Mkurugenzi Msaidiz wa Idara ya Habari MAELEZO, Zamaradi Kawawa akitoa neno la kuhitimisha mkutano huo.


IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA

MSIMAMIZI MKUU

KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV

0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

BREAKING NEWS | MKURUGENZI MTENDAJI WA TANESCO AFARIKI DUNIA

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE

#MAKINIKIA: HEKAYA FUPI YA MJI WA KIHISTORIA WA MOSHI MKOANI KILIMANJARO

HUU NDIO UKWELI ULIVYO RAFIKI YANGU

BODI YA LIGI SASA WAOMBA HEKIMA NA BUSARA ITUMIKE DERBY YA YANGA, SIMBA

RATIBA KAMILI YA HARUSI YA DIAMOND, ZUCHU

ZIJUE TABIA 9 ZA WANAWAKE HAWA....

TANZANIA NI MIONGONI MWA NCHI 10 ZINAZOONGOZA KWA MAZAO YA KILIMO AFRIKA