RC CHACHA AWATOA HOFU WALAJI WA ASALI YA TABORA ‎


 ‎Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paulo  Chacha amewatoa hofu walaji wa asali inayozalishwa mkoani humo kwamba iko safi, tofauti na inavyoenezwa kwamba ina kemikali ya Tumbaku.

‎Amesema kuwa  Ili kuepukana na  athari hiyo, Mkoa umetenga kwa umbali maeneo ya kilimo Cha Tumbaku na misitu ya uzalishaji wa  asali.

‎RC. Chacha amebainisha hilo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma Julai 11, 2025, kuhusu mafanikio ya miaka minne ya Mkoa huo katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

‎"Kawaida ya nyuki hawana uwezo wa kutafuta chakula umbali wa zaidi ya Km 5, ndiyo maana misitu ya kufugia nyuki imetenganishwa kwa umbali mrefu na mashamba ya tumbaku,"amesema RC Chacha.

‎Ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kwenda mkoani humo kuwekeza, kwani ipo misitu mingi inayofaa kwa ufugaji wa nyuki na kwamba asali ya Tabora ina ubora unaostahili.


IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 

0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MASIKINI

MAKUNDI YA VILABU VINAVYOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2025.

JINSI YA KUMTAWALA MWANAMKE HASA MKE (USIOE MKE WA MTU)

MUONEKANO WA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA MSALATO

DIARRA KIPA BORA TANZANIA

CHINYELE ACHUKUA FOMU KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE DODOMA MJINI