Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameongoza uzinduzi wa Mradi wa Maji katika Wilaya ya Longido, Julai 10 wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2025.
Aidha, Mhe. Kikwete amempongeza Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndg. Ismail Ali Ussi, pamoja na timu nzima ya wakimbiza mwenge kwa kazi kubwa na ya kizalendo wanayoifanya.
Amesema kupitia mbio hizo, vijana hao wameendelea kuhamasisha maendeleo, kueneza ujumbe wa matumaini kwa jamii, na kufika katika maeneo ambayo matumaini yalikuwa yameanza kufifia, hivyo kuamsha ari na mshikamano wa kitaifa.
Naye Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ali Ismail Ussi, amesema mwenge huo umekuwa chachu ya maendeleo nchini kwa kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali, ikiwemo mradi huu wa maji uliokamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Comments