- Get link
- X
- Other Apps
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Alliance for Democratic Change (ADC), Wilson Elias Mulumbe (katikati) aliyeambatana na Mgombea Mwenza, Shoka Khamis Juma (kushoto) katika tukio lililofanyika Agosti 14, 2025 Njedengwa jijini Dodoma.
Akizungumza na vyombo vya habari baada ya kuchukua fomu, Mgombea pendekezwa wa Urais wa chama hicho, Mulumbe amesema kuwa chama chake kikishinda atahakikisha anafuta madeni yote wanayodaiwa wanafunzi na Bodi ya Mikopo, itakuwa elimu bure, afya bure na wateja wataunganishiwa umeme bure.
Vyama vingine vilivyochukua fumu jana Agosti 13, 2025 ni; Chama cha Democratic Party (DP), Abdul Juma Mluya (Urais) aliyeambatana na Mgombea Mwenza, Masoud Abrahman Khatib na Chama cha Sauti ya Umma (SAU), Majalio Paul Kyara (Urais) aliyeambatana na Mgombea Mwenza, Satia Mussa Bebwa.
Vilivyochukua fomu Agosti 12, 2025 ni; Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD) ambacho mgombea wake urais ni Mwajuma Noty Mirambo aliyeambatana na Mgombea Mwenza, Mashavu Alawi Haji pamoja na Chama cha Tanzania Democratic Alliance ( ADA-TADEA), ambacho mgombea urais ni Georges Gabriel Bussungu aliyeambatana na Mgombea Mwenza, Ali Makame Issa.
Wagombea wengine waliochukua fomu Agosti 10, 2025 ni; Chama cha MAKINI ambacho wagombea wake ni Coaster Jimmy Kibonde. na Mgombea Mwenza, Aziza Haji Suleiman, National League for Democracy (NLD), Doyo Hassan Doyo (Urais) na Mgombea Mwenza, Chausiku Khatib Mohamed pamoja na United Peoples Democratic Party (UPDP), Twalib Ibrahim Kadege (Urais), Mgombea Mwenza, Abdalla Mohd Khamisi.
Vyama vilivyofungua pazia ya uchukuaji fomu Agosti 9, 2025 ni; Chama Cha Mapinduzi (CCM) mgombea wake wa Urais ni Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mgombea Mwenza, Dkt. John Nchimbi, Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA) walikuwa ni Hassan Kisabya Almas (Rais). na Mgombea Mwenza, Hamisi Ally Hassan pamoja na Chama cha Alliance for African Farmers Party (AAFP),Kunje Ngombale Mwiru (urais). Mgombea huyo wa AAFP aliambatana na Mgombea Mwenza, Shum Juma Abdalla.Hadi leo hii vyama vilivyochukua fomu ni 12.
Mulumbe akizungumza na vyombo vya habari baada ya kuchukua fomu.
Wafuasi wa chama hicho wakishangilia baada ya wagombea wao kuchukua fomu.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MSIMAMIZI MKUU
KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV
0754264203
HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI
RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI
WALIOKUWA WABUNGE WALIOPITIWA NA MKASI WA WAJUMBE
Watetezi wa majimbo yao walioanguka 1. Stela Manyanya (Nyasa) 2. Emmanuel Mwakasaka (Tabora Mjini) 3. Charles Kimei (Vunjo) 4. Deo Sanga (Makambako) 5. Antipas (Malinyi) 6. Nagindu Butondo (Kishapu) 7. Joseph Kakunda, (Skonge) 8. Ally Makoa (Kondoa Mjini) 9. Mwarami, 10. Amsabi Mrimi (Serengeti) 11. Benaya Kapinga (Mbinga) 12. Issa Chinguile (Nachingwea) 13. Doroth Kilave (Temeke) 14. Issa Mtemvu (Kibamba) 15. Hassan Mtenga (Mtwara Mjini), 16. Isack Francis Mtinga (Iramba Mashariki) 17. Innocent Bilakwate - Kyerwa 18. Assa Makanika (Kigoma Kaskazini) 19. Vita Kawawa (Namtumbo) 20. Jesca Msambatavangu (Iringa Mjini) 21. Anania Thadayo (Mwanga) 22. Atupele Mwakibete (Busekelo) 23. Joseph Ndaisaba (Ngara) 24. Cosato Chumi (Mafinga) 25. Joseph Kizito Mhagama (Madaba) 26. Maimuna Mtanda (Newala V) 27. Stanslaus Nyongo (Maswa Mashariki) 28. Marco John Sallu (Handeni Mjini) 29. Dkt. Daniel Pallangyo (Arumeru Mashariki) 31. Prof. Patrick Ndakidemi (Moshi Vijijini) 32. Exhaud K...
WALIOSHINDA KURA ZA MAONI CCM HAWA HAPA
O
SPIKA MSTAAFU NDUGAI AFARIKI DUNIA
Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania na Mbunge wa Kongwa, Job Yustino Ndugai amefariki Dunia leo August 06,2025 akiwa anaendelea kupatiwa matibabu Hospitalini baada ya kuugua ghafla. Kwa mujibu wa taarifa ya Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson aliyoitoa imesema: “Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika mstaafu wa Bunge, Job Ndugai kilichotokea leo jijini Dodoma. “Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Kongwa, Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.” Dk Tulia amesema Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na kamati ya mazishi pamoja na familia ya marehemu inaratibu mipango ya mazishi na taarifa zaidi zitaendelea kutolewa. Ndugai amekuwa Spika wa Bunge tangu November 17, 2015 hadi Januari 06, 2022 alipojiuzulu na kuendelea kuwa Mbunge wa Kongwa nafasi ambayo ameendelea kuitetea kwa kuchukua fomu tena mwaka huu ambapo ameshinda kwenye kura za maoni.
USAJILI ULIVYO HADI SASA....
1;Balla Mousa CONTÈ✅️ (Ashatambulishwa) 2;Mohammed DOUMBIA ✅️ (Bado utambulisho) 3;Lassine KOUMA✅️ (Bado utambulisho) 4;Celestin ECUA ✅️ (Bado utambulisho) 5;Andy BOYELI ⏳️(makubaliano yanaendelea) 6;Offen CHIKOLA ✅️(Ashatambulishwa) 7;Mohammed HUSSEIN MOHAMMED ✅️ Bado utambulisho) 8;Abdulnassir Mohammed ABDALLAH ✅️(Bado utambulisho) WANANCHI wanajipanga zaidi kuelekea mashindano ya kimataifa 🔥 Follow Yanga Pulse'#s 🙏🏾
RAIS SAMIA AYATAKA MASHINDANO YA MISS WORLD 2027
Tanzania yaitaka Miss World 2027! Dkt. Samia Afanya Mazungumzo Ndoto ya Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano ya kimataifa ya urembo, Miss World 2027, imechanua baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufanya mazungumzo muhimu na uongozi wa Kampuni ya Miss World Limited. Kikao hicho cha kihistoria kilifanyika Julai 20, 2025, huko Kizimkazi, Zanzibar. Uongozi wa Miss World Limited uliongozwa na Mwenyekiti na Mkurugenzi Mkuu wake, Bi. Julia Evelyn Morley, akiambatana na mshindi wa taji la Miss World 2025, Bi. Opal Suchata Chuangsri kutoka Thailand, pamoja na Miss World Africa, Bi. Hasset Dereje Admassu kutoka Ethiopia. Mazungumzo hayo, ambayo pia yalihudhuriwa na viongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, pamoja na viongozi wa Maliasili na Utalii, yalilenga kujadili namna Tanzania inavyoweza kuandaa kwa mafanikio makubwa mashindano hayo makubwa ya kimataifa. Mazungumzo haya kati ya Rais Dkt. Samia na uongozi wa Miss World yana...
MAMBO 7 MUHIMU YA KUYAEPUKA BAADA YA KUACHANA...
i. Kutafuta Mtu Mbadala Kwa Haraka Kabla Moyo Haujapona ii. Kufanya Mambo Ili Umuoneshe Kuwa Unaendelea Vizuri iii. Kuchukia Kila Mtu Hata Wasiohusika iv. Kufanya Mbinu Za Kumdhuru v. Kuhitimisha Hautapata Mtu Mwingine Kama Yeye vi. Kujingiza Kwenye Tabia Hatarishi Ili Kupoteza Mawazo vii. Kujiondolea Thamani Katika Makala Hii Tutazungumzia Jambo La Saba - Kujiondolea Thamani Kuachana na mtu kunaweza kukuondolea kabisa thamani yako unayojipa. Yaani unaweza kujiona kuwa hauna thamani tena na hakuna anaekutaka tena. Usisahau kuwa, unaweza kuachana na mtu na tatizo lisiwe kwako bali likawa kwake. Sio kila wakati unapoachana na mtu basi ni wewe haufai, inawezekana ni yeye ndiye hakufai. Usijihukumu na kujiondolea thamani. Wewe bado ni wa thamani na kuna wengi wanakuhitaji. Yaani, wewe ni ndoto ya watu fulani, wanatamani kukupata. Ndio ile msemo wa kiswahili wanasema... “Wakati mwingine anasema ni wa nini, kuna mwingine anajiuliza nitampata lini?” Th...
MWENYE MASIKIO NA ASIKIE....
# KWENYE #MAISHA #YAKO 1. Weka Mipaka ya Heshima (Set Boundaries): Sio kila mtu wa kumsaidia, sio kila mtu anastahili huruma yako. Tofautisha kati ya utu na kupuuzwa. 2. Jifunze Kusema “Hapana”: Ukitaka heshima, usiwe mtu wa ndiyo kwa kila jambo. Ukitumia nguvu zako hovyo, utamaliza heshima yako. 3. Jithamini Kabla Hujathamini Wengine: Usijitoe sadaka kwa watu ambao hata hawakuulizi unaendeleaje. Jiamini, jipende, jikubali. 4. Chagua Mpenzi Mwenye Moyo wa Kuthamini, Sio Kuokoa: Kama mwanamke ana majeraha ya zamani, hakikisha anajiponya mwenyewe. Usijaribu kuwa "daktari wa moyo wake" ukitegemea atakupenda zaidi. 5. Tafuta Misingi ya Maisha Yenye Malengo (Purposeful Living): Usijifungie kwenye kazi au mapenzi tu. Kuwa na maisha yenye dira: ndoto zako, afya yako, marafiki wa kweli. 6. Kua Kifedha na Kisaikolojia (Grow Financially & Emotionally): Jifunze uwekezaji, epuka utegemezi, weka akiba. Pia jifunze kujieleza, kusamehe, kujijenga kihisia. 7. Usikubali Uonevu Kazini a...
MWANAUME USIPITWE NA HILI, INASIKITISHA...?!!!
Kuna hali inazidi kushika kasi miongoni mwa wanaume wa kizazi hiki. Unakuta kijana anaonekana yupo sawa, ana tabasamu, ana marafiki, ana gari au hata ndoa lakini ndani yake kuna kilio kisichosikika, kuna mzigo Mkubwa usiobebeka, kuna uchovu wa kuishi maisha yasiyo yake. Mwanaume wa sasa amekuwa kama mchezaji wa maigizo. Anaigiza mafanikio, anaigiza furaha, anaigiza mapenzi yote ili aonekane yupo juu, awe na heshima mbele ya marafiki, aonekane “mwanaume wa maana” mbele ya jamii. Lakini ni wangapi wameangamia kwa sababu hiyo? Mashinikizo ya watu yamemweka mwanaume kwenye kona mbaya sana. Mwanaume anahisi hawezi kulalamika, hawezi kuomba msaada, hawezi kuanguka. Akilia anaitwa muoga. Akishindwa anaitwa dhaifu. Matokeo yake, anapigana na maisha peke yake mpaka anapotea kimya kimya. Depresheni inamla ndani kwa ndani, na hakuna anayejua. Leo hii kijana anaoa si kwa sababu ya upendo, bali kutimiza matarajio ya watu,jamii,washikaji,na marafiki. Anatafuta mwanamke “...
RAIS SAMIA AMUONDOLEA POLEPOLE HADHI YA UBALOZI
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Dk Samwel Shelukindo imeeleza kwamba, imepokea barua kutoka kwa Katibu Mkuu, Kiongozi Balozi Dk Moses Kusiluka ikitaarifu kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa mamlaka aliyo nayo chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ametengua uteuzi wa Humphrey Polepole, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba na kumuondolea hadhi ya ubalozi. Aidha, Rais Samia kwa mamlaka aliyonayo chini ya sheria ya utumishi wa umma amemuachisha kazi Polepole kwa manufaa ya umma.
Comments