Shangwe, shamrashamra zikiwa zimeupamba mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye viwanja vya Tambukaleli jijini Dodoma Agosti 31, 2025.
Baadhi ya ahadi alizozitoa mgombea huyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, Dkt Samia ambazo ziliwafurahisha wananchi wa Dodoma ni kulimaliza tatizo sugu la maji kwa kutoa maji kutoka ziwa Victoria na kukamilisha ujenzi wa bwawa kubwa la maji la Farkwa.
Mambo mengine ni kukamilisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato na kuanza ujenzi wa uwanja wa kisasa wa mpira utakaotumika wakati wa michuano ya AFCON Mwaka 2027.
IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA
MSIMAMIZI MKUU
KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV
0754264203







Comments