WMA YAENDELEA KUELIMISHA WANAFUNZI KUHUSU VIPIMO KUPITIA MAONESHO YA NANENANE

MENEJA wa Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa Wakala wa Vipimo (WMA), Bi. Veronica Simba,akitoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Brother Martin iliyopo  jijini Dodoma mara baada ya kutembelea banda la WMA katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA
WANAFUNZI  wa Shule ya Msingi Brother Martin ya jijini Dodoma wamepata fursa ya kujifunza kuhusu umuhimu wa vipimo sahihi, baada ya kutembelea banda la Wakala wa Vipimo (WMA) katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma.
Akizungumza na wanafunzi hao, Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma wa WMA, Bi. Veronica Simba, amesema kuwa  utoaji wa elimu ya vipimo kwa wanafunzi ni sehemu ya mkakati wa taasisi hiyo wa kufikisha uelewa wa vipimo sahihi kwa jamii kuanzia ngazi ya chini.
“Elimu ya vipimo ni msingi muhimu katika maisha ya kila siku, hasa katika shughuli za biashara na matumizi ya kila siku. Tunataka watoto wajifunze mapema kuhusu haki zao na namna ya kutambua vipimo sahihi ili wawe raia wanaotambua thamani ya usahihi na uadilifu,” amesema  Bi. Simba.

Katika kuhakikisha elimu hiyo inawafikia wanafunzi wengi zaidi, Wakala wa Vipimo umedhamiria kuanzisha vilabu vya vipimo katika shule mbalimbali nchini. Lengo ni kuwajengea wanafunzi msingi thabiti wa kuelewa masuala ya vipimo na kuwa mabalozi wa elimu hiyo katika jamii zao.

Maonesho ya Nanenane hutoa fursa kwa taasisi mbalimbali kuonesha huduma na bidhaa zao, huku pia yakiwapa wananchi nafasi ya kupata elimu ya kitaalamu kuhusu sekta mbalimbali ikiwemo vipimo, kilimo, afya na teknolojia.





Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

WALIOKUWA WABUNGE WALIOPITIWA NA MKASI WA WAJUMBE

MWANAUME USIPITWE NA HILI, INASIKITISHA...?!!!

USAJILI ULIVYO HADI SASA....

SPIKA MSTAAFU NDUGAI AFARIKI DUNIA

HUYU NDIYE MWANAMKE WA KUOA

RAIS SAMIA AYATAKA MASHINDANO YA MISS WORLD 2027

MWENYE MASIKIO NA ASIKIE....

MAMBO 7 MUHIMU YA KUYAEPUKA BAADA YA KUACHANA...