ZUNGU APITISHWA NA CCM KUGOMBEA USPIKA WA BUNGE

Mbunge Mteule wa Ilala, Mussa Azzan Zungu amechaguliwa kwa kishindo kuwa Mgombea wa Spika la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi uliomalizika  Dodoma leo Novemba 9, 2025.

 Zungu ambaye alikuwa Naibu Spika amepata Kura  348 akimshinda mpinzani wake Stephen Masele aliyepata kura 16. 

Mbunge Mteule wa Babati Vijijini, Daniel Sillo amechaguliwa kuwania Unaibu Spika kupitia Chama hicho kwa kupata kura 362. Aliokuwa akigombea nao walijitoa.

Uchaguzi wa Spika na Naibu Spika wa Bunge utakaoshirikisha wagombea wengine kutoka vya  upinzani utafanyika katika kikao cha kwanza cha Mkutano wa Bunge wa 13 baada ya wabunge wateule kuapishwa.

Uchaguzi huo wa ndani ya CCM ambao wapiga kura walikuwa wabunge wote wateule wa Chama hicho, ulifunguliwa na Katibu Mkuu wa Chama hicho,  Balozi Asha-Rose Migiro na kusinamiwa na Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, John Mongella.

Spika anayemaliza muda wake ambaye pia alijitoa kwenye kinyang'anyiro hicho, Dkt Tulia Ackson alishuhudia uchaguzi huo.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

WALIOCHUKUA FOMU CCM ZA KUWANIA USPIKA HAWA HAPA

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

RAIS SAMIA SIO RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI, TANZANIA SIO KENYA

MJUE VIZURI KOCHA MPYA WA YANGA PEDRO

MATOKEO YA DARASA LA 7 YATANGAZWA

JESHI LA POLISI LATEKELEZA AGIZO LA RAIS SAMIA, LAONDOA KIZUIZI CHA KUTOTOKA NJE BAADA YA SAA 12 JIONI