DKT. KIKWETE AKABIDHIWA KITABU CHA MWALIMU NYERERE CHA 'JAMHURI NA PLATO'

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea nakala ya kitabu “Jamhuri na Plato” kilichotafsiriwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kutoka kwa Bw. Walter Bgoya, Mkurugenzi wa kampuni ya uchapishaji ya Mkuki na Nyota, mwishoni mwa juma jijini Dar es Salaam.

Kitabu hiki, asili yake ikiwa ni The Republic (Politeia) cha mwanafalsafa wa Kigiriki Plato, kinajadili mazungumzo ya Socrates, ambapo Plato anachambua aina za tawala, asili ya nafsi, nadharia ya maumbo na dhana ya mji bora (Kallipolis) unaoongozwa na wanafalsafa-wafalme. 

Tafsiri hii ya Mwalimu Nyerere inaleta fikra hizi karibu na muktadha wa Afrika, ikisisitiza maadili, uongozi wenye hekima na wajibu wa raia katika kujenga jamii bora.


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

BODABODA ALIPWA PIKIPIKI BAADA KUSAFIRI KWA BODA KWA SAA 10 MBEYA HADI DAR

ASANTE GWIJI YAYA TOURE KWA KUPASUA UKWELI UKWELI KUPENDELEWA KWA MOROCCO

CONFIRMED HAWA NDIO WACHEZAJI WETU 12 WA KIGENI 🦾

RAIS WA SENEGAL AWAPATIA ZAWADI NONO WACHEZAJI WALIOFANIKISHA UBINGWA WA AFCON 2025

NYOMI YA WASENEGALI WAKISHANGILIA UBINGWA WA AFCON 2025

'MAREKANI IKIJARIBU KUANZISHA VITA NA URUSI ITAANGAMIA'

Wasifu wa Kizza Besigye

TANZANIA YAPANDA VIWANGO VYA FIFA