SERIKALI KUANZISHA MFUKO MAALUMU WA KUPUNGUZA MAKALI YA BEI YA MAFUTA

SERIKALI imeamua kuanzisha Mfuko Maalumu utakaosaidia kupunguza makali ya bei ya mafuta ambayo imepanda kufuatia vita vinavyoendelea kati Israel, Marekani na Irani.

Mpango huo umeelezwa na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari katika Makao Makao ya CCM.jijini Dodoma Aprili 7, 2026.

Amesema kuwa CCM na Serikali itahakikisha mafuta yanapatikana wakati wote na kwa bei nafuu.

Aidha, Kihongosi amesema kuwa  Serikali pia ina mpango wa kutoa ruzuku katika mafuta kama ilivyofanya wakati wa vita vya Urusi na Ukraine ambapo Serikali ilitoa  bil. 100.


 IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA - 0715264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

KATI YA WATOTO 7 WA HAYATI MAGUFULI ANAYEJULIKANA ZAIDI NI JESCA

KIKOSI KILICHOITWA TAIFA STARS HIKI HAPA

KWA KHERI MAKARANGA UMEUTIMIZA MWENDO...

UBORA UNAONEKANA: BENKI YA NMB YANG'ARA TUZO ZA EUROMONEY 2026

WANAJESHI WAGOMA KWENDA IRAN KUPIGA

MCHIMBAJI MDOGO WA DHAHABU AFANYA MAKUBWA KWENYE HUDUMA ZA AFYA