NMB YAWAPA WAFANYABIASHARA MBINU ZA UKUAJI ENDELEVU



Benki ya NMB imeendelea kuimarisha huduma kwa wafanyabiashara kupitia NMB Business Club, jukwaa linalowapa wateja elimu ya fedha, teknolojia na fursa mbalimbali za kukuza biashara zao kwa uendelevu. Semina hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Cardinal Rugambwa, Dar es Salaam.

Akizungumza katika semina hiyo, Mwenyekiti wa NMB Business Club Mkoa wa Dar es Salaam na Mjumbe wa Bodi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Award Mpandila, alisema jukwaa hilo limekuwa muhimu kwa kuwaunganisha wafanyabiashara na kuwajengea uwezo wa kutumia mifumo rasmi ya kifedha. Aliwahimiza wafanyabiashara kupitisha mauzo yao kupitia benki ili kujenga historia nzuri ya kifedha inayoweza kuwasaidia kupata huduma mbalimbali, ikiwemo mikopo.
Kwa upande wake, Meneja Mwandamizi wa Business Banking Benki ya NMB, Reynold Tony, alisema benki hiyo itaendelea kutoa bidhaa, elimu na suluhisho zinazolenga kuimarisha biashara za wateja wake. Alisema NMB inalenga kuwa mshirika wa karibu wa wafanyabiashara katika kujenga biashara imara na zinazoweza kukabiliana na mabadiliko ya soko.

Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria, akiwemo Eileen Kunaga na Ally Kuburi kutoka Ilala, walisema jukwaa hilo limewasaidia kupata elimu kuhusu matumizi ya sola, usimamizi wa fedha na huduma za taasisi mbalimbali, ikiwemo TRA. Walisema maarifa hayo yanaweza kupunguza gharama za uendeshaji na kusaidia biashara kukua kwa muda mrefu.









 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MSALATO DODOMA KUANZA KUTUMIKA SEPTEMBA 2026

BALOZI WA CHINA KUPITIA DKT. MAJULE APELEKA NEEMA KWA WANAWAKE DODOMA

SERIKALI YAINGIA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO NA DIT KUIMARISHA USIMAMIZI WA MAAFA

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

BREAKING NEWS…!! SERENGETI BOYS WAVUNJA KAMBI NA VILIO KIBAO

USIYO YAJUA KUHUSU ANGE KAGAME