MBUNGE DKT. MDAKU AFADHILI MAFUNZO YA MUZIKI KWA WANAMUZIKI WA BENDI YA MALINYI

Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Malinyi, Mhe. Dkt. Mecktridis Mdaku, inawapongeza vijana wote wa Bendi ya Muziki ya Malinyi waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya kozi ya muziki na sanaa.

Tunawataka wanufaika wote waliotajwa kufika kwa wakati katika Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi cha Victory siku ya Jumamosi, tarehe 01 Agosti 2026, ili kuanza rasmi mafunzo yaliyodhaminiwa na Mheshimiwa Mbunge.

Hii ni hatua muhimu ya kuwawezesha vijana kukuza vipaji vyao, kujenga taaluma, na kufungua fursa mpya katika sekta ya sanaa na muziki.

Hongereni kwa wote mliochaguliwa. Tunawatakia mafanikio mema katika safari yenu ya kujifunza na kutimiza ndoto zenu.



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

OWM–TAMISEMI YASHINDA TUZO YA MABADILIKO YA KIDIJITALI KATIKA TEHAMA AWARDS 2026

NI MAKOSA WANAFUNZI KUFIKA SHULE SAA 1:15 ASUBUHI

MAFAO YA MAKAMU WA RAIS ALIYEJIUZULU

VIONGOZI NA WATENDAJI WA MATAWI UVCCM PANGANI WANOLEWA

NMB YAWAUNGANISHA WANANCHI NA HUDUMA, FURSA ZANZIBAR