RAIS DKT SAMIA MGENI RASMI UZINDUZI WA MRADI WA KUZALISHA NISHATI YA UMEME RUFIJI AGOSTI 22

Na Victor Masangu,Pwani 

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu  Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za uzinduzi wa mradi mkubwa wa kimkakati wa Bwawa la kuzalisha umeme wa maji la Mwalimu Julias Nyerere  lililopo kata ya Mloka  Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani siku  Agosti 22 mwaka huu.

Akizungumuza na waandishi habari ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge amesema kwamba   kituo hicho  cha kina uwezo wa kuzalisha   megawati za umeme zipatazo elfu  2,115 kupitia mitambo tisa  iliyokamilika na kuunganishwa na gridi ya Taifa na kwamba kwamba maandalizi yote yanakwenda vizuri.

 
Aidha katika hatua nyingine  Mkuu huyo wa Mkoa amesema kwamba serikali imejipanga vilivyo katika suala zima la ulinzi na usalama na kuwahimiza wananchi kuhakikisha wanalinda vyanzo vya maji ikiwemo mradi wa Bwawa hilo ambalo ni mkombozi mkubwa katika kuleta chachu ya kiuchumi na maendeleo kwa  wanannchi wa maeneo mbali mbali.


Rais Samia atazindua Bwawa hilo huku mataifa makubwa duniani yakipigwa na butwaa kwa namna ambavyo Tanzania imeweza kukamilisha Bwawa hilo chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Bwawa la kufua Umeme la Mwalimu Nyerere (JNHPP) ni uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya Tanzania kwa kutumia fedha zake za ndani  kiasi cha Sh.Trilioni 7.452 ambapo ujenzi wake ulianzishwa na Rais wa awamu ya tano Hayyat John Pombe Magufuli.


 
Kukamilika kwa mradi wa kuzalisha umeme  wa Bwawa la Mwalimu Julias Nyerere lililopo Wilaya ya Rufiji Mkoa wa Pwani  utaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa nchi nzima kupitia gridi ya Taifa  ikiwemo baadhi ya  Mikoa ya Pwani, Morogoro, Dar es Salaam, Mkoa wa Lindi pamoja na mikoa mingine
.                                               



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

OWM–TAMISEMI YASHINDA TUZO YA MABADILIKO YA KIDIJITALI KATIKA TEHAMA AWARDS 2026

VIONGOZI NA WATENDAJI WA MATAWI UVCCM PANGANI WANOLEWA

NMB YAWAUNGANISHA WANANCHI NA HUDUMA, FURSA ZANZIBAR

HIZI HAPA TAKWIMU ZA PETER SHALULILE MCHEZAJI MPYA WA YANGA SC ๐Ÿ”ฐ ๐Ÿ”ฅ

KAMATI YA BUNGE PAC YABAINI MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA UMMA MZUMBE