‎WAHITIMU 62,680 WA TIA WAINGIA SOKO LA AJIRA, UJASIRIAMALI

 JUMLA  ya wanafunzi 62,680 wamehitimu katika Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa mwaka 2025/2026 na kuingia katika soko la ajira, ujasiriamali na kutoa huduma mbalimbali za kitaaluma

Afisa Mtendaji Mkuu wa TIA, Prof. William Pallangyo alisema mafanikio ya TIA hayapimwi kwa ongezeko la idadi ya wanafunzi na kampasi pekee, bali pia kwa idadi ya wataalamu wanaozalishwa na kuingia katika soko la ajira.

‎.Alisema takwimu hizo zinaonesha mchango wa TIA katika kuzalisha rasilimali watu yenye ujuzi unaohitajika katika utekelezaji wa shughuli za kiuchumi na maendeleo ya Taifa.

‎“Ukuaji wa TIA haujikiti tu katika idadi ya wanafunzi, bali unaendelea kutengeneza rasilimali watu inayohitajika katika uchumi wa Taifa letu,” alisema.

Alisema katika mwaka wa fedha 2026/27, TIA itaendelea kuimarisha programu za elimu, kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu ya juu na kuwekeza katika mazingira bora ya kujifunzia ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya elimu ya uhasibu, biashara, uchumi na maeneo mengine yanayohusiana na taaluma hizo.

Prof. Pallangyo alikuwa akielezea utekelezaji wa TIA katika mwaka wa fedha 2025/26 pamoja na mwelekeo wa taasisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27, katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari–MAELEZO, jijini Dodoma.


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

OWM–TAMISEMI YASHINDA TUZO YA MABADILIKO YA KIDIJITALI KATIKA TEHAMA AWARDS 2026

MATUKIO MBALIMBALI WAKATI WA KUAPISHWA NDEJEMBI KUWA MAKAMU WA RAIS

MAFAO YA MAKAMU WA RAIS ALIYEJIUZULU

NI MAKOSA WANAFUNZI KUFIKA SHULE SAA 1:15 ASUBUHI

URUSI, CHINA, IRANI NA KOREA KASKAZINI WAPANGA KUUNDA JESHI MOJA LA KUJIHAMI

PANYA MAGAWA WA SUA TANZANIA AJENGEWA MNARA WA HESHIMA CAMBODIA