MUSOMA VIJIJINI WAMPONGEZA RAIS SAMIA KUTOA FEDHA ZA UJENZI WA DARAJA NYABATIRYA+video


                                Rais Samia Sluhu Hassan


Wafanyabiashara wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan  na serikali kwa ujumla kutoa sh. mil. 41 ya kugharamia ujenzi wa Daraja kwenye Mto Nyabatirya, Musoma vijijini.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti wafanyabiashara hao wamesema kuwa ujenzi wa daraja hilo umesaidia kwa kiasi kikubwa  kutatua changamoto iliyokuwa inawakabili ya usafiri wa kuunganisha Vijiji 3 vilivyoko kwenye Mwambao wa Ziwa Victoria.


DARAJA hilo limewezesha BIADHAA za UVUVI & KILIMO kusafirishwa kwa urahisi.


Aidha, wafanyabiashara hao wametoapongezi kubwa kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo kwa juhudi kubwa za kuwapigania wananchi kuhakikisha  jimbo hilo linapiga hatua za kimaendeleo katika sekta ya elimu, afya na miundombinu.


Tafadhali sikiliza MAELEZO, MAONI na SHUKRANI za WANAVIJIJI na KIONGOZI wa TARURA kwenye "CLIP" iliyoambatanishwa hapa.


Taarifa kutoka:

*Ofisi ya TARURA

Musoma DC

*Ofisi ya Mbunge

Jimbo la Musoma Vijijini

www.musomavijijini.or.tz



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

RAIS SAMIA SIO RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI, TANZANIA SIO KENYA

MJUE VIZURI KOCHA MPYA WA YANGA PEDRO

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA

BALOZI MIGIRO AKUTANA NA JOPO LA WAANGALIZI WA UCHAGUZI MKUU WA UMOJA WA AFRIKA