MUSOMA VIJIJINI WAMPONGEZA RAIS SAMIA KUTOA FEDHA ZA UJENZI WA DARAJA NYABATIRYA+video


                                Rais Samia Sluhu Hassan


Wafanyabiashara wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan  na serikali kwa ujumla kutoa sh. mil. 41 ya kugharamia ujenzi wa Daraja kwenye Mto Nyabatirya, Musoma vijijini.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti wafanyabiashara hao wamesema kuwa ujenzi wa daraja hilo umesaidia kwa kiasi kikubwa  kutatua changamoto iliyokuwa inawakabili ya usafiri wa kuunganisha Vijiji 3 vilivyoko kwenye Mwambao wa Ziwa Victoria.


DARAJA hilo limewezesha BIADHAA za UVUVI & KILIMO kusafirishwa kwa urahisi.


Aidha, wafanyabiashara hao wametoapongezi kubwa kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo kwa juhudi kubwa za kuwapigania wananchi kuhakikisha  jimbo hilo linapiga hatua za kimaendeleo katika sekta ya elimu, afya na miundombinu.


Tafadhali sikiliza MAELEZO, MAONI na SHUKRANI za WANAVIJIJI na KIONGOZI wa TARURA kwenye "CLIP" iliyoambatanishwa hapa.


Taarifa kutoka:

*Ofisi ya TARURA

Musoma DC

*Ofisi ya Mbunge

Jimbo la Musoma Vijijini

www.musomavijijini.or.tz



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MASIKINI

MAKUNDI YA VILABU VINAVYOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2025.

JINSI YA KUMTAWALA MWANAMKE HASA MKE (USIOE MKE WA MTU)

MUONEKANO WA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA MSALATO

DIARRA KIPA BORA TANZANIA

CHINYELE ACHUKUA FOMU KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE DODOMA MJINI