Rais Samia Sluhu Hassan
Wafanyabiashara wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan na serikali kwa ujumla kutoa sh. mil. 41 ya kugharamia ujenzi wa Daraja kwenye Mto Nyabatirya, Musoma vijijini.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wafanyabiashara hao wamesema kuwa ujenzi wa daraja hilo umesaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto iliyokuwa inawakabili ya usafiri wa kuunganisha Vijiji 3 vilivyoko kwenye Mwambao wa Ziwa Victoria.
DARAJA hilo limewezesha BIADHAA za UVUVI & KILIMO kusafirishwa kwa urahisi.
Aidha, wafanyabiashara hao wametoapongezi kubwa kwa Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo kwa juhudi kubwa za kuwapigania wananchi kuhakikisha jimbo hilo linapiga hatua za kimaendeleo katika sekta ya elimu, afya na miundombinu.
Tafadhali sikiliza MAELEZO, MAONI na SHUKRANI za WANAVIJIJI na KIONGOZI wa TARURA kwenye "CLIP" iliyoambatanishwa hapa.
Taarifa kutoka:
*Ofisi ya TARURA
Musoma DC
*Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
Comments