MADAKTARI WALIPAMBANA KWA NGUVU ZOTE KUMNUSURU JENISTA MHAGAMA IKASHINDAKANA- MCHENGERWA

Kumbe Jenista Aliumwa Akazidiwa Dodoma                                                                                     Waziri wa Afya, Mohammed Mchengerwa, amefichua kuwa licha ya jitihada kubwa zilizofanywa na madaktari wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kuokoa maisha ya aliyekuwa Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama, hali yake ilikuwa mbaya sana alipowasili hospitalini hapo na baadaye alifariki dunia.

Akizungumza leo Jijini Dodoma, nyumbani kwa marehemu Itega, Mchengerwa amesema alipokea taarifa kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kwamba madaktari walipambana kwa nguvu zote tangu walipompokea marehemu, lakini licha ya juhudi hizo, Mungu alimchukua.

“Nichukue fursa hii kuwashukuru madaktari wote waliomhudumia pale Benjamin Mkapa. Walifanya kazi kubwa sana mpaka dakika za mwisho ambapo Katibu Mkuu alinifahamisha kuwa hali yake ilikuwa mbaya sana na baadaye Mwenyezi Mungu akamchukua,” amesema Mchengerwa.

Aidha, Waziri Mchengerwa amewataka madaktari wa hospitali hiyo kuendelea kuwa na moyo wa kutoa huduma bora kwa wagonjwa wengine kama walivyofanya kwa marehemu Jenista Mhagama.

Vilevile, ameahidi kuwa Wizara ya Afya itaendeleza na kutekeleza maono, dira na miradi aliyoiacha Jenista Mhagama mara baada ya kumkabidhi kijiti cha uongozi ndani ya wizara hiyo hivi karibuni.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

HUYU NDIYE WANU HAFIDH, CHAMPIONI WA ELIMU

MAWAZIRI WALIOACHWA HAWA HAPA

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

𝐌𝐉𝐔𝐄 𝐊𝐀𝐂𝐇𝐄𝐑𝐎 𝐌𝐙𝐄𝐍𝐀

HISTORIA YA MAREHEMU MC PILIPILI

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...

NAPE AWAPA UKWELI VIJANA