ALAT MKOA WA MARA WASHUHUDIA USHIRIKIANO MZURI KATI YA WANANCHI NA SERIKALI YETU KWENYE UJENZI WA KIGERA SEKONDARI
Jumatano, 17.4.2024, Viongozi wa ALAT Mkoa wa Mara walitembelea Kigera Sekondari iliyojengwa Kijijini Kigera (Etuma), Kata ya Nyakatende.
Sekondari hii ambayo ni ya pili ya Kata ya Nyakatende, ilianza kujengwa Mwaka 2020 kwa nguvu za Wananchi wa Vijiji viwili vya Kigera (Etuma) na Kakisheri, na Mbunge wao wa Jimbo la Musoma Vijijini.
Baadae, Serikali ilichangia na inaendelea kuchangia ustawi wa shule hii. Miumbombinu ya Elimu ya Sekondari hii imejengwa kwa ubora mkubwa - ALAT imedhibitisha ubora huu!
Tafadhali sikiliza CLIP/VIDEO iliyoambatanishwa hapa - Wananchi wanashukuru sana juhudi za Serikali yetu.
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Musoma Vijijini
www.musomavijijini.or.tz
P. O. Box 6
Musoma
Tarehe:
Alhamisi, 18.4.2024
Comments