RC ANDENGENYE AKAGUA UTEKELEZAJI MIRADI YA NYONGEZA ITOKANAYO NA BARABARA YA KABINGO, KASULU MANYOVU

 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye amewataka wakandarasi wanaotekeleza miradi ya nyongeza kutoka mradi Mkuu wa Barabara ya Kabingo, Kasulu hadi Manyovu yenye urefu wa Km. 260 kukamilisha miradi hiyo kwa wakati ili kuendana na malengo ya serikali katika kuharakisha utoaji wa huduma kwa wananchi.


Andengenye amesema hayo akiwa wilayani Buhigwe kwenye ziara yake ya kukagua miradi hiyo inayotekelezwa kwa Thamani ya Shilingi Bil. 20 katika wilaya za Buhigwe, Kasulu na Kibondo ambapo miradi hiyo inahusisha ujenzi wa Masoko, Stendi, Miundombinu ya Maji, Elimu na uboreshaji wa vituo vya kutolea huduma za Afya.


Amesema wakandarasi hao wanapaswa kuzingatia makubaliano yao na serikali ili kuhakikisha miradi hiyo ya nyongeza inakamilika sambamba na ujenzi wa barabara ya Kabingo, Kasulu hadi Manyovu.


Upande wake Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Kigoma Mha. Narcis Choma amesema kupitia utaratibu huo, katika wilaya ya Buhigwe inatekelezwa Miradi ya ujenzi wa Soko la Mnanila, stendi ya mabasi Buhigwe, matanki ya kuhifadhi Maji katika vijiji vya Bweranka na Kibwigwa pamoja na ujenzi wa Shule ya Sekondari Kidato cha Tano na Sita Buhigwe.


Mha. Choma amesema miradi hiyo itakapokamilika wananchi wataona thamani ya ziada ya utekelezaji wa miradi ya barabara katika maeneo yao ikiwemo ujenzi na maboresho ya miundombinu mbalimbali ya kutolea huduma za jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye akikagua miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa Thamani ya Shilingi Bil. 20 katika wilaya za Buhigwe, Kasulu na Kibondo ambapo miradi hiyo inahusisha ujenzi wa Masoko, Stendi, Miundombinu ya Maji, Elimu na uboreshaji wa vituo vya kutolea huduma za Afya.












Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAMBO YANAYOUA NDOA NA MAHUSIANO

RAIS SAMIA ANA KWA ANA NA ZUHURA YUNUS

JINSI YA KUMSAHAU EX WAKO ALIEKUACHA;

USHAURI WA BURE KWA KILA MFANYAKAZI

JINSI BINTI HUYU MWANAFUNZI ANAVYOIPENDA MITI

TAKUKURU YAPONGEZWA KUWA BEGA KWA BEGA NA MBIO ZA SEPESHA ZINAZOPINGA RUSHWA YA NGONO

NDOGO WA MUME WANGU ALIKUWA EX WANGU