AUWSA YAUNGANISHA MAJI ZAIDI YA KAYA 6000 MASIKINI ARUSHA


 Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Arusha (AUWSA),  Mhandisi Justine Rujomba amesema kuwa Mamlaka hiyo imewezesha zaidi ya kaya  masikini 6000 zimeunganishiwa maji kwa gharama nafuu ya sh. 30,000 kwa Kila kaya.

Pamoja na mambo mengine, ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari -MAELEZO jijini Dodoma Machi 14, 2025, kuhusu mafanikio ya Mamlaka hiyo kuelekea maadhimisho ya miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Mhandisi Rujomba amesema kuwa AUWSA imevunja  rekodi kwa kutoa huduma ya maji kwa asilimia 99 badala ya asilimia 95 inayotakiwa kufikiwa ifikapo 2025 kwa mujibu wa utekekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MSIMAMIZI MKUU 
KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV
 0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

RAIS TRUMP ARARUANA NA RAIS WA UKRAINE

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

SERIKALI YALIKUBALI OMBI LA DIAMOND

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

ARAJIGA AULA KOMBE LA DUNIA