TANTRADE YATANGAZA MAFANIKIO LUKUKI AWAMU YA RAIS SAMIA


 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TANTRADE), Bi. Latifa M. Khamis, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio na mwelekeo wa mamlaka hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita leo Machi 13, 2025, katika Ofisi za Idara ya Habari - MAELEZO, jijini Dodoma.

Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.



MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU KWA MWAKA 2023/2024 NA 2024/2025

Katika kipindi hiki, TanTrade imefanikiwa kupanua masoko, kusaidia biashara za Tanzania kupata fursa za kimataifa, kujenga uwezo wa wafanyabiashara wadogo na wa kati, na kuboresha mifumo ya upatikanaji wa taarifa za biashara.

 

 

 

1.1 Kuratibu na Kusimamia Mifumo ya Soko la Ndani

Katika eneo hili, Mamlaka imetekeleza mambo yafuatayo;

 

a.    Uratibu wa DITF ambao ulipelekea mafanikio yafuatayo kwa kipindi cha mwaka 2020/21 -2023/24:

                i.        Washiriki wa ndani wameongezeka kutoka 2,926 hadi 3,503, huku washiriki wa nje wakiongezeka kutoka 76 hadi 451.

              ii.        Nchi zinazoshiriki zimeongezeka kutoka 17 hadi 28.

             iii.        Watembeleaji wa maonesho wamefikia zaidi ya 300,701.

             iv.        Ajira za muda mfupi zimeongezeka kutoka 11,200 hadi 11,869.

              v.        Mauzo ya papo kwa papo yamefikia shilingi bilioni 3.62.

             vi.        Fursa za mauzo kupitia maonesho zimefikia thamani ya shilingi bilioni 25.16

            vii.        Mikataba ya kibiashara yenye thamani ya shilingi bilioni 176 ilisainiwa, ongezeko kubwa kutoka shilingi bilioni 5.6

 

b.    Hati za Makubaliano (MoU) zenye thamani ya shilingi bilioni 17 zilisainiwa kupitia Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya China (CIIE) 2023/24

 

c.    Expo 2020 Dubai

                            i.        Kusainiwa kwa (MoU) 36 za makubaliano zenye thamani ya Dola Bilioni 7.49 (Tshs. Trilioni 17.35).

                          ii.        Ajira 200,000 zilipatikana.

                         iii.        Washiriki 640 wa Kitanzania walihudhuria.

                         iv.         Watembeleaji 928,469 kutoka nchi mbalimbali duniani walitembelea sehemu ya maonesho ya Tanzania (Tanzania Pavillion).   

 

d.    Maonesho ya Mbogamboga Expo Doha, 2023/24

                      i.        Kampuni 13 zilishiriki na kufanikisha mauzo ya papo kwa papo ya shilingi milioni 370.

                    ii.        Fursa za mauzo za shilingi milioni 125 zilifunguliwa kupitia mazungumzo ya kibiashara.

                   iii.        Kampuni za Qatar zilionesha nia ya kuwekeza katika usindikaji wa chakula na usimamizi wa taka.

e.     Maonesho ya Biashara ya Afrika (AfCFTA Exhibitions on Intra-Africa Trade) ya mwaka 2023 ambapo: -

                            i.        Mauzo ya papo kwa papo yenye thamani ya TZS bilioni 2.17 yalifanyika.

                          ii.        Mikataba ya biashara yenye thamani ya TZS bilioni 17 ilisainiwa.

 

1.1  Kutoa mafunzo na ushauri kwa sekta binafsi hususani Wafanyabiashara

TanTrade imeendelea kuwajengea uwezo wafanyabiashara wadogo na wa kati kwa kuwawezesha kushindana katika masoko ya ndani na nje kupitia mafunzo ya biashara.

a.    Programu 37 za mafunzo zimeratibiwa, zikihusisha wafanyabiashara 3,556. Mada zilizofundishwa katika kipindi cha miaka minne ni pamoja na:

                                i.        Usimamizi na uendeshaji wa biashara (washiriki 922)

                              ii.        Mbinu za kufikia masoko ya ndani na nje (washiriki 630)

                             iii.        Taratibu za kuuza nje na uelewa wa mfumo wa taarifa za biashara (washiriki 253)

                             iv.        Mafunzo kwa wafanyabiashara wa mipakani (washiriki 51).

 

b. Katika kipindi cha miaka minne mafanikio yafuatayo yalipatikana kupitia Kliniki za biashara;

                                i.        Jumla ya wafanyabiashara 3,256 walihudumiwa kupitia kliniki zilizofanyika katika maonesho na mikutano ya kibiashara.

                              ii.        Jumla ya changamoto 1,324 ziliwasilishwa, ambapo 1,298 zilitatuliwa, na 26 zipo katika hatua za utekelezaji, hususan zinazohusiana na mitaji na vibali vya biashara.

                             iii.        Kampuni 482 zilipatiwa msaada wa usajili kupitia taasisi wezeshi kama BRELA, BPRA, na TRA, na biashara mpya zilianzishwa.

                             iv.        Kampuni 137 zilisaidiwa kupata ushauri alama za ubora, vifungashio vinavyokidhi viwango vya soko la kimataifa, na mbinu za kuongeza thamani ya bidhaa.

                              v.        Wafanyabiashara 238 waliunganishwa na wanunuzi wa ndani na nje ya nchi kupitia mikutano ya B2B na B2G, ambapo biashara za bidhaa kama asali, mazao ya nafaka, mbogamboga, na viungo zilifanikishwa.

                             vi.        Wafanyabiashara 312 walipatiwa mafunzo kuhusu mbinu bora za biashara, taratibu za forodha, na miongozo ya kodi kupitia TRA.

 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

RAIS TRUMP ARARUANA NA RAIS WA UKRAINE

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

SERIKALI YALIKUBALI OMBI LA DIAMOND

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

ARAJIGA AULA KOMBE LA DUNIA