VIONGOZI WA BENKI YA NMB WAHUDHURIA UZINDUZI WA DIRA YA TAIFA 2050

Viongozi wa Benki ya NMB wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, CPA. David Carol Nchimbi,(Kulia) wakiwa ndani ya Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC) jijini Dodoma, wakifuatilia kwa makini hafla ya uzinduzi wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Uzinduzi huo umefanyika leo chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, sekta binafsi pamoja na wadau wa maendeleo kutoka ndani na nje ya nchi.

Benki ya NMB, kama mshirika mkuu wa maendeleo ya kiuchumi nchini, imeonesha dhamira yake ya kuunga mkono utekelezaji wa Dira hii mpya inayolenga kuifikisha Tanzania katika hatua za juu za maendeleo jumuishi, shindani na endelevu ifikapo mwaka 2050.


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MASIKINI

MWANAUME USIPITWE NA HILI, INASIKITISHA...?!!!

HUYU NDIYE MWANAMKE WA KUOA

DIARRA KIPA BORA TANZANIA

MAKUNDI YA VILABU VINAVYOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2025.

CHINYELE ACHUKUA FOMU KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE DODOMA MJINI