Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira amewakumbusha watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo kushirikiana na Wanahabari ili wananchi waweze kufahamu mambo mbalimbali yahusuyo Uchaguzi.
Wito huo ameutoa leo alipokuwa akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo yaliyofanyika kwa siku tatu katika Kituo cha Tabora yaliyojumuisha watendaji kutoa Mikoa wa Tabora na Kigoma.
"Katika utekelezaji wa majukumu yenu, mtapaswa kutoa taarifa mbalimbali kwenye vyombo vya habari ili kuwajulisha wananchi na wadau wa Uchaguzi mambo mbalimbali yanayohusu Uchaguzi" alisema Mhe.Rwebangira.
Aidha Mhe.Rwebangira amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha wanatunza rasilimali vifaa vya Uchaguzi watavyovipokea kwaajili ya Uchaguzi sambamba na kuhakikisha wanafuata Sheria, kanuni na miongozo kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili wakatimizie jukumu la usimamizi wa Uchaguzi kwa weledi.
Mafunzo haya ya siku tatu yenye lengo la kuwajengea uwezo watendaji wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 yamekamilika leo tarehe 17 Julai, 2025.
Comments