KATIBU MKUU WA CCM, BALOZI DKT. MIGIRO AKUTANA NA RAIS MWINYI – ZANZIBAR

Leo, tarehe 8 Septemba 2025, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amekutana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Ikulu Zanzibar.

Katika mazungumzo hayo, Dkt. Migiro amemfikishia Dkt. Mwinyi salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia ni Mgombea wa Urais kupitia CCM, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Dkt. Migiro amempongeza Dkt. Mwinyi kwa kuaminiwa tena na kuteuliwa na Chama kuwa Mgombea wa Urais wa Zanzibar.

#KaziNaUtuTunasongaMbele
#OctobaTunatiki






 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

NENO KUNTU LA UMMY MWALIMU ALILOLITOA BAADA YA KUTEMWA KUGOMBEA UBUNGE

WAGOMBEA WALIOENGULIWA CCM LICHA YA KUONGOZA KURA ZA MAONI

CHONGOLO AMKUMBUKA DKT. ASHA-ROSE MIGIRO-

RC KIHONGOSI AELEZA MAFANIKIO LUKUKI MKOA ARUSHA

WALIOKUWA WABUNGE WALIOPITIWA NA MKASI WA WAJUMBE

MBINU ZITAKAZOKUFANYA USIISHIWE PESA