SHANGWE ZARINDIMA DKT. SAMIA AKIKUBALI KUUPANDISHA HADHI MJI WA MBALIZI.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan amelikubali ombi la kuupandisha hadhi Mji mdogo wa Mbalizi kuwa Halmashauri ya Mji.



Amesema kuwa endapo mchakato ndani ambao umeanza ukifikishwa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) basi wao kama serikali wataangalia ni jinsi gani ya kuipandika hadhi Mbalizi kuwa Halmashauri ya Mji.


Dkt. Samia ametoa majibu hayo liyopokelewa kwa shangwe na wananchi wa mji huo baada ya kuombwa na Mbunge Mteule wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Patali Shida Patali  wakati wa mkutano wa kampeni za mgombea huyo urais uliofanyika leo Septemba 4, 2025 kwenye viwanja vya Mlima Reli Mbalizi mkoani Mbeya.







Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

WALIOKUWA WABUNGE WALIOPITIWA NA MKASI WA WAJUMBE

NENO KUNTU LA UMMY MWALIMU ALILOLITOA BAADA YA KUTEMWA KUGOMBEA UBUNGE

SPIKA MSTAAFU NDUGAI AFARIKI DUNIA

WAGOMBEA WALIOENGULIWA CCM LICHA YA KUONGOZA KURA ZA MAONI

CHONGOLO AMKUMBUKA DKT. ASHA-ROSE MIGIRO-