𝙈𝙖𝙩𝙪𝙨𝙞 𝙣𝙞𝙖𝙘𝙝𝙞𝙚𝙣𝙞 𝙢𝙞𝙢𝙞, 𝙣𝙞𝙣𝙖𝙮𝙖𝙗𝙚𝙗𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙣𝙞𝙖𝙗𝙖 𝙮𝙚𝙣𝙪.
"..Niwahakikishie tarehe 29, kesho kutwa tu mwezi huu wa 10, niwaombe tokeni muende mkapige kura."
"Ninayeongea hapa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii, ninataka niwaambie, maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kwenda vituoni kupiga kura, hakuna maandamano mengine yatakayokuwepo hapa.."
"..hakuna tishio la kiusalama litakalokuwepo, anayesemahapa ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi hii."
"Niwaombe ndugu zangu, twendeni mkapige kura, twendeni mkapige kura... Ndugu zangu mengine niachieni mimi, matusi niachieni mimi, ninayabeba kwa niaba yenu"
"Niliapa kuwa Rais wa Tanzania, niliapa kuilinda Nchi hii kwa kudumisha Amani, Umoja na Mshikamano wetu"
Hayo yamesemwa na Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 wakati akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo tarehe 21 Oktoba 2025.
Comments