KAMPENI ZA DKT. SAMIA KURINDIMA BUZA DAR LEO

Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Rais Dkt Samia Suluhu Hassan leo zinafanyika Buza Tanesco wilayani Temeke, Dar es salaam baada ya kufanikisha katika Wilaya za Ubungo, Kinondoni na Ilala.

Kampeni za leo zitashirikisha Wilaya mbili za Temeke na Kigamboni zenye majimbo manne ya uchaguzi ya Temeke, Chamazi, Mbagala na Kigamboni.

Baada ya kuhitimisha kampeni leo kwa Mkoa wa Dar es salaam, Dkt. Samia  atavuka Bahari ya Hindi kwenda kwenda kuomba kura Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar na hatimaye kufunga Kampeni Rocky City Mwanza.

‎Akiwa katika mikutano hiyo, Dkt. Samia hujinadi kwa kuelezea mafanikio makubwa ya miradi ya maendeleo yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika  mikoa 26 ya Tanzania Bara na mitano ya Tanzania Visiwani, pia hutoa ahadi ya utekelezaji wa miradi mbalimbali kwa miaka mingine mitano endapo atashinda katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 29.

‎Aidha, Dkt. Samia amekuwa akisisitiza kudumisha Muungano na kuendelea kulinda amani na utulivu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

‎Pia amewatoa wananchi wasiwasi kwamba hakutokuwa na vurugu  kwani vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko imara, hivyo siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29 mwaka huu  wajitokeze kwa wingi tena bila hofu kwenda kupiga kura na kurejea salama majumbani.

‎Pamoja na kuelezea kwa undani Ilani ya uchaguzi ya chama hicho, Dkt. Samia ambaye mgombea wake mwenza ni Dkt. Emmauel Nchimbi, hutumia fursa hiyo kujinadi yeye,  wagombea ubunge na madiwani wa chama hicho.

‎IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA-0754264203



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

KIGOGO WA CHADEMA AHAMIA CCM

RAIS SAMIA SIO RAIS JOYCE BANDA WA MALAWI, TANZANIA SIO KENYA

RAIS SAMIA AMZAWADIA NYUMBA SIMBU