KATIBU MKUU RAMEPRO, BONIVENTURA MWALONGO AKISAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO CHA MAREHEMU KARDINALI PENGO

Kwa masikitiko makubwa na huzuni nzito, tumepokea taarifa ya kifo cha Mwadhama Polycarp Cardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Marehemu alikuwa mchungaji mwaminifu na kiongozi mwenye hekima na busara, aliyelitumikia Kanisa na Taifa kwa uaminifu mkubwa, akiacha alama isiyofutika katika mioyo ya wengi.

Kwa niaba yangu binafsi na kwa niaba ya Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO), ninawasilisha salamu za rambirambi kwa Kanisa Katoliki, familia ya marehemu, waumini wote, na Watanzania wote walioguswa na msiba huu mkubwa katika Kanisa na Taifa letu.

Tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, apumzike kwa amani ya milele.

“Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alikuwa kama sisi, nasi tutakuwa kama yeye; hivyo tujiandae.”

Imetolewa na:
Boniventura Mwalongo
Katibu Mkuu – TRAMEPRO

Tarehe: 24 Februari 2026



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

MBUNGE DKT. MAJULE ATOA MSAADA WA VYAKULA, VYANDARUA 100 SHULE YA VIZIWI DODOMA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

MAMBO MADOGO YANAYOVUTIA KWA MPENZI WAKO

DKT. MAJULE AKABIDHIWA CHETI CHA SHUKRANI UWT DODOMA KUFANIKISHA USHINDI WA CCM 2025

30 TANZANIAN PROJECTS IN THE NEXT 10 YEARS

PUNGUZA STRESS....