Tanzania Investment and Special Economic Zones Authority (TISEZA) imewasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kuendeleza Kampeni ya Kitaifa ya Uhamasishaji Uwekezaji wa Ndani hatua inayolenga kuwasha ari mpya ya Watanzania kuchangamkia fursa za kiuchumi.
Ziara hiyo ni awamu ya pili kwa Nyanda za Juu Kusini baada ya kukamilika kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa, huku mamlaka hiyo ikitembelea miradi inayomilikiwa na wazawa ili kuhamasisha uwekezaji, kutoa elimu kuhusu vivutio vya kikodi na visivyo vya kikodi, na kusisitiza kipaumbele kinachotolewa kwa wawekezaji wa ndani.
Akizungumza wakati wa mapokezi, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Beno Malisa amesema Mbeya ni lango muhimu la biashara kwa nchi za Southern African Development Community (SADC), akibainisha kuwa mkakati sahihi unaweza kuwafanya wafanyabiashara wengi kuchagua kuwekeza Mbeya badala ya kuelekea Kariakoo.
#WekezaMbeya #FursaZaNdani #BiasharaBilaMipaka



Comments